Tuesday 16 December 2014

Only Bongo land you can be congratulated and blamed by the President !

The Bongoland attorney general was forced to resign after giving the country bad advice and squander billions of shillings . The President give him kudos for good work and bad advice and enjoy his retirement but not facing any charge for Escrow Blander  which cost Tanzania economy ! This is how CCM cosmetic work you steal billions and transfer you to another ministry or Embassy with out justice be done to the country , Let wait and see Kikwete tough Uamuzi in few days and See Tubaijuka with few others named by parliament transferred to another positions in Nyerere party style ! 


Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia leo, Jumanne, Desemba 16, 2014 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amekubali ombi hilo la kujiuzulu.  Katika barua yake kwa Mhe. Rais Kikwete, Jaji Werema amesema kuwa ameomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusiana na suala ya Akaunti ya Tegeta Escrow hakueleweka na umechafua hali ya hewa.  Mhe. Rais Kikwete amemshukuru Jaji Werema kwa utumishi wake ulioongozwa na uaminifu na uadilifu.



"Mheshimiwa Spika, Kamati imepitia Mkataba wa mauzo ya Hisa kati ya Kampuni ya PAP na VIP na kuthibitisha kuwa Waziri wa Nishati na Madini Mheshimiwa Prof. Sospeter Muhongo (Mb) ndiye alikuwa kiungo kati ya Bw. Harbinder Singh Sethi wa IPTL na Ndg. Rugemalira wa VIP (Kiambatisho Na. 16). Katika mkataba huo wa tarehe 19 Agosti, 2013. Ndg. James Rugemalila alithibitisha kuwa Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof. Sospeter Muhongo alimwomba kuwasilisha kiasi cha fedha ambacho angependa kulipwa na IPTL ili kumaliza Shauri lililokuwepo mahakamani. Aidha, Bw. Sethi aliwasilisha kwa Bw. Rugemalira ushahidi kwamba PAP imenunua Hisa 7 za Mechmar katika IPTL. “On 11th July 2013, the Minister of Energy and Minerals, Hon. Dr. Prof. Sospeter Muhongo invited VIP to submit to him the amount of money if paid VIP would conclusively settle VIP claims against IPTL”Mheshimiwa Spika, mchakato wote wa kutoa fedha katika Akaunti ya Tegeta ESCROW ndipo ulipoanza na mauzo ya hisa za VIP kwenda PAP na baadaye kuhitimishwa na maamuzi ya Mahakama Kuu ya tarehe 5 Septemba, 2013 ambayo ndiyo yaliyotumika kuhalalisha utoaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta ESCROW tarehe 28 Novemba hadi 5 Desemba, 2013" - UKURASA WA 58 WA 'TAARIFA YA KAMATI [YA KUDUMU YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)] KUFUATIA MATOKEO YA UKAGUZI MAALUM WA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KATIKA AKAUNTI YA TEGETA ESCROW ILIYOKUWA KATIKA BENKI KUU YA TANZANIA'

"Mheshimiwa SpikaKutokana na tofauti zilizokuwepo kati ya MECHMAR na VIP kuanzia mwanzo wa mradi, VIP iliamua kuuza Hisa zake zilizoko IPTL kwa makampuni mbalimbali kwa nyakati tofauti ikiwemo MECHMAR kama mwanahisa mwenzake, NSSF, Camel Oil, Great White Shark Opportunity Fund pamoja na SYMBION lakini haikuwezekana kutokana na kutoafikiana katika bei. Mheshimiwa SpikaBaadaye VIP chini ya usuluhishi ya RITA, iliuza Hisa zake kwa PAP kwa thamani ya Dola za Marekani milioni sabini na tano (US$ 75,000,000/=). Ununuzi wa Hisa Asilimia 30 za VIP uliofanywa na PAP ndiyo uliyomaliza mgogoro wa Wanahisa uliyokuwa Mahakamani na kuufanya Mtambo wa IPTL kumilikiwa na PAP kwa kuwa ndiyo iliyomiliki Hisa zote Asilimia 100 za IPTL. Taarifa ya PAC: Katika ukurasa wa 58 wa Taarifa ya PAC imeelezwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini ndiye aliyekuwa Dalali Mkuu aliyewakutanisha Bw Harbinder Sethi na Bw James Rugemalira     Ufafanuzi Mheshimiwa Spika, Taarifa hii siyo sahihi kwa kuwa tangu tarehe 9 Novemba, 2011, RITA aliitisha mkutano na kuwakutanisha wadau wote wa IPTL. Wakati huo, Waziri wa Nishati na Madini aliyeko sasa alikuwa bado hajateuliwa kwenye wadhifa huo"  - UKURASA WA 11-12 WA 'UTETEZI WA SERIKALI' KUPITIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI

"Tarehe 15 Agosti 2013 kampuni ya VIP iliingia makubaliano na PAP ya kuuza hisa tatu (3) katika IPTL, ambapo utekelezaji wa makubaliano hayo ulianza rasmi tarehe 19 Agosti 2013 kulingana na Kipengele Na. 1.26 cha Makubaliano ya Uuzaji na Ununuzi wa Hisa hizo (Kielelezo 65 ). Wakati wa makubalino hayo yanafanyika kampuni ya IPTL ilikuwa katika ufilisi. Mahakama Kuu ya Tanzania iliridhia (taking judicial notice) makubaliano haya katika hukumu ya tarehe 5 Septemba 2013" - UKURASA WA 29 WA 'TAARIFA YA UKAGUZI MAALUM [WA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) KUHUSIANA NA MIAMALA ILIYOFANYIKA KATIKA KAUNTI YA 'ESCROW' YA TEGETA, PAMOJA NA UMILIKI WA KAMPUNI YA IPTL ILIYOWASILISHWA NA CAG KWA KATIBU WA BUNGE.'

No comments: