Thursday 25 June 2015

LIPUMBA ASUBIRIWA KAMA ALMASI HUKO KANDA YA ZIWA, NDIYO! NI MWANZA MARA HII NA MAENEO JIRANI.WANANCHI WASEMA NI TUMAINI PEKEE LA WATU WA KANDA HIYO NA TANZANIA KWA UJUMLA, WASEMA WAMECHOKA KULA MAPANKI KUTOKANA NA UGUMU WA MAISHA.


Mwenyekiti wa chama cha wananchi cuf taifa mheshimiwa Prof Ibrahim Haruna Lipumba jumamosi hii anatarajiwa kuwasili mkoani MWANZA kwa ziara ya kichama kwa zaidi ya mwezi mzima.
"Ninakwenda MWANZA na kanda nzima ya ziwa kuwakumbusha ndugu zangu kujiandikisha kwa wingi ktk bvr lakini pia kuwajulisha kuwa mapanki wanayokula si ridhiki toka kwa mungu wao bali no laana ya kuikumbatia ccm kwa zaidi ya miaka 50"
"Mapanki ni chakula wanachostahili kula mifugo na kama kuna matumizi ya ziada ya mapanki ni utengenezaji wa mbolea viwandani"
Lakini kutokana na ugumu wa maisha yanayotokana na Sera mbovu jumlisha wizi wa mali za umma usiyo na mfano na ufisadi uliokithiri ndiyo maana ata wao wakazi wa kanda hiyo wanashindwa kula sangara safi, sato mzuri na neema nyingine nyingi za ziwa victoria kutokana na ugumu wa maisha uliosababishwa na chama hicho licha ya kuwa samaki hao wapo ktk eneo jirani na makazi badala yake wananchi wa eneo hilo akitaka kula samaki basi anakwenda kununua mifupa ya samaki hao na kufanya ndoyo mboga huku minofu ya samaki hao ikienda nje kwa wazungu"
"Jambo la kushanga ata baada ya samaki hao kwenda nje kodi inayotokana na minofu hiyo bado wajanja wanagawana na kusema eti 10ml ni pesa ya mboga"

" Nataka kuwambia watu wa MWANZA na watanzania kwa ujumla kwa majaaliwa ya mwenyezi mungu nikijaaliwa kuiongoza nchi yetu baada ya kunipa kura zao kwa wingi ninawakikishia mafisadi wote wanafilisiwa mali zao zilizo ndani na nje ya nchi, mafisadi wote wataishia jela siyo leo mafisadi papa na nyangumi wanagombania kuenda Dodoma kuchukua form za kugombea urais loh!"
"Nataka niwaeleze watu wa MWANZA kuwa serikali yangu itaakikisha inaurejesha mchakato wa kupatikana kwa katiba huru kwa mujibu wa maoni yao yaliyo kusanywa na jaji warioba na siyo ile ya kaka yangu sita na mwenzake ambaye kila deal la ufisadi nchini hakosekani"
Alimaliza kusema bingwa huyo wa uchumi dunia alipokuwa akizungumza na wanachama wa chama chake leo buguruni.
Wakati huo huo timu tayari imeshatangulia ktk uwanja wa mapambano huko MWANZA ikiongozwa na mkurugenzi wa habari, Sera uenezi na mahusiano kwa umma mweshimiwa Abdul Kambaya na tayari wameshafanya mikutano kadhaa ktk mkoa huo na mwingine ukiwa unaendekea hivi sasa.
Hakiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii!?
KAJIANDIKISHE KWENYE BVR KISHA TUKUTANE 25/10/2015.
KATAA CCM FUTA NA DELETE KABISA.

No comments: