Sunday 10 April 2016

Udhaifu wa JK, siyo uimara wa JPM

Rais Jakaya KIkwete (kulia) akifurahi na Rais mteule, John Magufuli muda mchache baada ya kutangazwa kushinda uchaguzi
MPAKA sasa, sifa kuu ya Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Rais John Magufuli ni kujenga ufuasi wa kushangiliwa kwa kila jambo, Washangiliaji wako kila kona. Wapo kwenye mitandao ya kijamii, wapo mitaani na hata kwenye mikusanyiko ya watu.Kimsingi, uimara wa Rais Magufuli unaoonekana kuwepo, unatokana na udhaifu wa awamu iliyopita.Shangwe na vigelegele vinavyopigwa leo kwa Rais Magufuli, zinatokana na mchoko wa muda mrefu waliokuwa nao wananchi, hususan katika kipindi chote cha miaka kumi ya utawala wa rais aliyepita, Jakaya Kikwete.Kinachofanyika sasa, ni ukali na kujenga hofu kwa watumishi wa umma. Serikali hii imeanza kujenga kasumba mbaya kwa wananchi.
Serikali inajikosha na kujenga hisia bandia kwa wananchi kwamba, matatizo yao hayatokani na serikali yenyewe, bali watendaji wa serikali.Ni hatari sana, kwa serikali kuanza kujenga hisia za uchonganishi kwa watendaji dhidi ya wananchi.Orodha ya matukio ya namna hii ni ndefu. Leo madaktari na wauguzi hawako salama kazini. Baadhi ya maeneo wameanza kutishia kogoma kutoka na vitisho na vipigo wanavyopata kutoka kwa ndugu na jamaa wa wagonjwa.

Ni hatari sana kumwaminisha na kuhadaa wananchi kuwa, huduma mbovu za kijamii wanazopata, hususan katika hospitali zetu, zinatokana na madaktari na wauguzi kuiba dawa.
Ukiwasikiliza wauguzi na madaktari wanasema, “huwezi kuiba dawa ambazo hazipo.” Serikali inawachonganisha watendaji wake kwa wananchi ili ipumue. Sijawahi kuona!
Kuna mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii kwa sasa kuhusu mshahara wa rais. Kama kawaida, Rais Magufuli anamiminiwa sifa kemkem kwa kuweka mshahara wake hadharani.
Yaleyale, wanaoshangilia na kupiga vigelegele, wanamulinganisha Rais Magufuli na mtangulizi wake, Kikwete. Ukweli ni kwamba, udhaifu wa Kikwete hauwezi kuwa uimara wa Rais Magufuli.
Uzalendo wa rais haupimwi kwa kutangaza mshahara wake. Bali tunahitaji rais asiyependa kupiga dili wala kufanya biashara akiwa ikulu.
Hatutaki rais anayeweza kujificha kwenye kivuli cha dola ili kudhoofisha wapinzani wake na wanaokosoa serikali.
Kasumba inayojengwa kwa kasi hivi sasa ni kwamba, yeyote anayekosoa na kutoa maoni mbadala, anaonekana kama mkorofi na siyo mzalendo.
Uzalendo siyo uzuzu wa kukaa kimya. Wala uzalendo haupimwi kwa kukubali kila kitu kinachosemwa na watawala.
Katika taifa ambalo ubabe unaitwa ujasiri na udhaifu wa kutofuata sheria na taratibu, unaitwa uungwana, huko ni kutengeneza wazalendo wa kuchonga.
Baada ya sakata la Zanzibar, hasa kwenye vituko vya kuamua kurejea uchaguzi Machi, 20, 2016, na Rais Magufuli akasema hahusiki na wala hana uwezo wa kuingilia utata ulioibuka uchagzi wa visiwa hivyo, vikiwa sehemu ya muungano wa Tanzania, inaonekana nchi inaendeshwa kibabe, haifuatwi matakwa ya wananchi na kiongozi mkuu anakubali kuisigina Katiba.
Pamoja na hilo la Zanzibar kusimamiwa kibabe na hatimaye kupita, bado Rais Magufuli amebakiza changamoto kadhaa.
Kwanza, mchakato uliokwama wa Katiba Mpya. Wapo baadhi ya viongozi waandamizi katika serikali hii ya Rais Magufuli wanaojipanga kimkakati kukwamisha hoja ya kufufua mchakato wa katiba mpya.
Nilimsikia waziri mmoja mwandamizi akisema, “wananchi mahitaji yao siyo Katiba Mpya, bali huduma bora za kijamii na kuboreshewa maisha yao.” Hawa ndio wanaomzunguka Rais Magufuli.
Hawa ndio washauri wakuu wa rais. Rais Magufuli asijifiche kwenye koti la washauri. Ajifunze kwa mtangulizi wake. Mambo yakienda kombo anayemiminiwa shutuma ni rais, siyo washauri.
Pili, kivuli cha Kikwete ndani ya Serikali ya Magufuli. Kinachoelezwa kuwa ni “utumbuaji wa majibu” ndani ya awamu hii ya tano, kinaenda sambamba na upangaji safu wa awamu hii.
Rais Magufuli anataka kujenga safu yake mpya atakayofanya nayo kazi. Kikwazo pekee ni kuwa, huwezi kupata safu mpya bila uwepo wa chembechembe za masalia ya Kikwete.
Mzee mmoja mashuhuri ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ameonya kuwa, kama Rais Magufuli atapewa kuwa Mwenyekiti wa CCM, basi asiwategemee wanaCCM kumsaidia katika harakati zake za “utumbuaji majipu”.
Sababu ni kwamba, baadhi ya wabunge wa CCM ndio wametuhumiwa na hata kufikiswa mahakani kwa mashitaka ya rushwa.
Kwa hiyo, Bunge haliwezi tena kuwa chombo cha kuibua uozo na tuhuma za rushwa, kwa sababu sehemu ya Bunge hilo, liko kwenye kashfa. Mnara wa kutunga sheria unapotuhumiwa, usitegemee mijadala mikali ndani ya bunge kuhusu ufisadi wala tuhuma zingine zinazofanana na hizo.
Hivyo, Rais Magufuli hawezi kupata msaada kutoka kwa wabunge wa CCM ndani ya Bunge. Na pia sasa mhimili wa Bunge, umepoteza sifa za kuwajadili mafisadi.
Huu ni mkwamo mwigine kwa Rais Magufuli, hususan kwa wabunge wa CCM wenye idadi kubwa na kuwa na uwezo wa kufanya uamuzi ndani ya Bunge, ambao una maslahi ya chaa chao na serikali.
Rais Magufuli mwenyewe anaweza kuwa changamoto. Hulka yake ya kutopenda kuamini kila mtu na kusimamia uamuzi wake mpaka mwisho hata kama siyo sahihi, inaweza kuchochea changamoto zaidi.
Hulka ya kutoamini kila mtu ina madhara yake. Hasara yake ni kujenga watendaji na wasaidizi wasiojiamini, wao wanasubiri kauli ya rais, ndipo wachangamke na kutenda kwa uoga.
Orodha ya matukio ya namna hii ni mengi. Wapo wanaoogopa kufanya uamuzi ambao upo ndani ya uwezo wao, kwa mujibu wa sheria na taratibu, lakini hawafanyi hivyo kwa hofu ya kukosea na kumkera bwana mkubwa.
Matokeo yake kazi haziendi mpaka tamko la Ikulu, tena kutoka kwa mkuu wa nchi liwafikie. Hawawezi kuwa wabunifu na kuamua ili kazi ziende kasi na maendeleo ya wananchi kupatik

No comments: