Monday 13 April 2015

LIPUMBA NA WAFUASI WAKE WAPATA DHAMANA UPYA

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar ambaye pia ni Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Hamad akisalimiana na Mwenyekiti wake Prof. Lipumba baada kutoka katika chumba cha kesi.

Wakifurahia jambo nje ya mahakama.MWENYEKITI wa chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba,  na wanachama wenzake ambao mwanzo walifunguliwa kesi ya kushiriki maandamano haramu,  wamepewa dhamana  upya katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Dhamana hiyo imetokana na  kesi yao ya awali ambayo ilifutwa na kuanza kupitiwa upya.
Wafuasi wa CUF wakiwa nje ya mahakama.
…Wakitawanyika baada ya wafuasi wao kupewa dhamana.
MWENYEKITI wa chama cha CUF, Profesa Ibrahim Lipumba,  na wanachama wenzake ambao mwanzo walifunguliwa kesi ya kushiriki maandamano haramu,  wamepewa dhamana  upya katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Dhamana hiyo imetokana na  kesi yao ya awali ambayo ilifutwa na kuanza kupitiwa upya.
Katika kupewa dhamana upya, watuhumiwa  hao japokuwa walikuwa nje kwa dhamana,  walitakiwa kufika leo na wadhamini wawili kila mmoja na kusaini karatasi ya maandishi yenye kiasi cha thamani ya Shilingi milioni mbili kila mmoja.
Watuhumiwa wote walikidhi vigezo.
Pia, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad,  alihudhuria mahakamani hapo na kusema amefurahishwa na kitendo cha hakimu kwa kuwapatia dhamana watuhumiwa wote.
‘’Nimefurahishwa na kitendo cha hakimu kufuata sheria na kuhakikisha watuhumiwa wamepata dhamana na hata wadhamini wao kujitokeza,” alisema.
 Mwendesha Mashtaka wa kesi hiyo, Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Cyprian Mkeha,  alitaja shauri hilo kusikikilizwa tena Mei 6.  Watuhumiwa wote wanakabiliwa na kosa la kutaka kufanya mkutano na maandamano pasipokuwa na kibali.

No comments: