Friday 6 August 2021

TANZANIA YAVUNJA REKODI KUPATA GAIDI WA KWANZA ASIE MUISLAMU KULIKONI ?

 *"UGAIDI  WA  MASHEIKH  MIAKA   YOTE  USHAHIDI  HAKUNA,  LAKINI  "UGAIDI  WA  MBOWE  USHAHIDI TAYARI   NA KESI CHAPUCHAPU  KULIKONI?*



*Masheikh  waachiwe  huru  polisi  ikipata  ushahidi  iwalete  mahakamini*


*MAONI YA Sauti  ya  wazalendo  halisi  Africa* 


Kwa  mara  ya  kwanza  mtuhumiwa  wa  kesi  ya  ugaidi  asiyekua  Muslimu  apatikana Tanzania.


Mh  Freeman  Mbowe  mwenyekiti  wa  chama  cha  upinzani  Chadema  amekabiliwa  na  tuhuma  za  ugaidi.


Dunia  imemshuhudia  kamanda  wa  jeshi  la  Polisi Mh  IGP  Simoni  Siro  mbele  ya  vyombo  vya  habari  akitamba kuwa: "Jeshi  la Polisi lina  ushahidi  wa  kutosha  na  ushahidi  umekamilka  Kwa  tuhuma  za  Mh  Mbowe."'

Dunia inataka kuaminishwa vijana watatu waliokuwa walinzi wa Mheshimiwa Mbowe amabo wote ni waislamu kuwa Waislam uwa Tanzania wanahusishwa na ugaidi hili kwa Waislamu wa Tanzania wanatakiwa wafikiri zaidi nini kitakachoendela kupikwa na utawla wa CCM dhidi ya Waislamu 


_Dunia  imepata  mshangao  mkubwa  sana  kumbe  jeshi  la  polisi  linaweza  Kupata  ushahidi  wa  tuhuma  za  ugaidi  kwa  haraka  hivo  na  kesi  kuanza  kwenda  chapuchapu kiasi  hicho  mpaka  kwa  njia  ya  mtandao? ????.?_


Kwanini  jeshi  la  polisi  limekosa  ushahidi  wa  tuhuma  za  ugaidi  kwa  Masheikh, Maimamu na Waalimu wa Madrasa  Zaid  ya  200. waliojazwa  mahabusu  mbalimbali  za  Tanzania kwa zaidi  ya  miaka  Mitano kwa madai upelelezi  haujakamilika  na hata  mahakamini  hawapelekwi  tena  kwa  muda  mrefu na  hakuna  uhakika  kama  upelelezi  huo  unaendelea!!.


Wazalenzo  halisi   Africa tunakuomba  Mh  Kamanda  Siro  ujitokeze  tena  mbele  ya  dunia  kupitia  vyombo  vya  habari  uieleze  dunia  Kwanini  uliwakamata  masheikh  ili  Hali  hauna  ushahidi  wa  makosa  yao? ??


Njoo  Kamanda  Siro  uieleze  Dunia  Kwanini  umeshindwa  kuthitibisha  tuhuma  za  ugaidi  kwa  Masheikh  kwa  miaka  Mitano  na  Zaidi  na  bado  unaendelea  kuwashikilia? ??


*Je  waislamu  wakisema  imetungwa  sheria  ya  ugaidi  kupambana  na  uislamu  Watakuwa  wamekosea? ????*


Waislamu  wakisema  jeshi  la  polisi  linatumia  vibaya  sheria  ya  ugaidi  kupambana  na  waislamu  je  watakua  wamekosea? ?????


Ikiwa  leo  masheikh  Zaidi  ya  200  kwa  miaka  Zaidi ya  mitano  mumewapa  tuhuma  za  ugaidi  lakini  hadi  sasa  hakuna  ushahidi  je  huku  sio  kutumia  kivuli  cha  ugaidi  kuwakomoa  waislamu? ??


Wazalenzo  halisi  Africa hatujasahau  mauaji  ya  imamu  aliyekuwa  mwanafunzi  wa  chuo  kikuu  alipouawa kwa  kupigwa  risasi  akipita  bank wilayani  Temeke  eneo  la  mtoni  na  kesho  yake Mh  Siro  uliitangazia  dunia  kuwa  imamu  Salumu  alikua  gaidi  kwasababu  alisikika  akisema  "Allah  akbar"


Haukupita  muda  Mh  Siro  ukapanda  cheo  kuwa  IGP kutoka  kuwa  RPC  wa  mkoa  wa  Dsm, bado  kuna  maswali  mengi  sana  kifo  cha  Imamu  Salumu  na  Tamko  la  kamanda  Siro  ndiyo  limempandisha  cheo  au  kitu  gani? ???


Na  je  ilifaa  kweli kumpandisha  cheo  mara  baada  ya  kuwajeruhi  waislamu  waliokua  Wana  uchungu  wa  mwenzao  kuuawa  na  Kamanda  Siro  kuhalalisha  kifo  cha  imamu  Salumu  kwakusema  Allah akbar? ???????


Wazalendo  halisi  wanatoa  wito  kwa  jeshi  la  polisi  kujitokeza  Tena  hadharani  kuitangazia  dunia  kuwa  haijapata  ushahidi  wa  tuhuma  za  ugaidi  za  masheikh  na  hivo  waachiwe  huru.


Wazalenzo  halisi  wanalipongeza  jeshi  la  polisi  kufanya  uchunguzi  haraka  kwa  tuhuma  za  Mh  Mbowe  na  kuipeleka  kesi  haraka Haraka  mpaka  kwa  njia  ya  mtandao  ili  imalizike  haraka 


Lakin  wazalendo  halisi  wanahoji  kwanini  jeshi  la  polisi  limeshindwa  kufanya  haraka  hiyo  kwa  masheikh wenye  tuhuma  kama  za  Mh  Mbowe? ????


Wazalendo  halisi  wanahoji  au  kwakuwa  wale  masheikh  ni  waislamu? 

Washatkiwa,, watatu wanaoshtakiwa na Mbowe wote ni Waislamu isipokuwa Mbowe itabidi kwa hili tumbadili jina mheshiwa Mbowe tumuite, Mheshimiwa Hamisi Mbowe kuonesha jinsi ugaidi unavyosingiziwa kwa Waislamu wa Tanzania. 

Imekuaje uchunguzi wa Mheshimiwa Hamisi Mbowe umekamilika kama miujiza?

Waislamu wa Tanzania kwa hili la ugaidi wanatakiwa wafikiri kwa mapana.


Au  kwakuwa  mataifa  ya  nje  ikiwemo  Marekani  wameanza  kuinyoshea  kidole  nchi yetu  ?


Je  jeshi  la  polisi  linataka  waislamu  pia  waanze  maandamano  yasiyoisha  kushinikiza  kuachiwa  masheikh  ndiyo  kesi  itaenda  na  ushahidi  utakuwa  tayari? ?

Pia kulikoni waislamu wamegawanywa kwa mafungu baina ya  Waislamu wa bara na wa Zanzibar wale masheikh wa Zanzibar wameonekana hawana hatia hawa wa huku kwetu wanaozea magerazani?


*#WAACHIWE  MASHEIKH,  AACHIWE  MH  MBOWE  WAWE  HURU  WOTE  SIO  MAGAIDI#*


*Sauti  ya  wazalendo  halisi*

No comments: