Sunday 26 July 2015

Madaktari kutoka Marekani watembelea chuo cha Afya Zanzibar


Madaktari Diaspora kutoka Marekani wakitowa Huduma ya Elimu kwa Wanafunzi wa Chuo cha Eilimu ya Afya Kuhusiana na Saratani ya Matiti na Meno.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora Zanzibar Ndg Adila Hilal Vuai, akiutambulisha Ujumbe wa Madaktari Diaspora kutoka Washington walioletwa na Jumuiya ya Watanzania Wanaoishi Washington wakali walipofika katika Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar walipofika hapo kutowa Elimu ya Afya ya Saratani ya Matiti na Mano, wakiwa Zanzibar kwa uwenyeji wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ)

Rais wa Jumuiya ya Watanzania Washinton Ndg Iddi Sandaly akiutambulisha Ujumbe wa Madaktari 17 Diaspora, waliofika Zanzibar kutoa Tiba ya Maradhi ya Saratani ya Matiti, Kisukari na Meno akitowa maelezo wakati walipofika katik Chuo cha Elimu ya Afya Mombasa Zanzibar, na kutowa Elimu ya kutambua Saratani ya Matiti kwa Kinamama. na kutowa huduma ya uchunguzi wa Meno.
Rais wa Jumuiya ya Wanawake Afrika Washington (Africa Womens Cancer Awereness Association ) Dr Ify Anne Nwabukwu, akiutambulisha ujumbe wa Madaktari wa maradhi mbalimbali waliowasili Zanzibar kwa ajili ya kutowa huduma kwa wananchi wa Zanzibar ikiwa ni kusaidia Wafrika wenzao walioko Afrika.

Rais wa Jumuiya ya Wanawake Afrika Washington (Africa Womens Cancer Awereness Association ) Dr Ify Anne Nwabukwu, akiutambulisha ujumbe wa Madaktari wa maradhi mbalimbali waliowasili Zanzibar kwa ajili ya kutowa huduma kwa wananchi wa Zanzibar ikiwa ni kusaidia Wafrika wenzao walioko Afrika. Wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar wakimsikiliza Dr Ify akitowa maelezo na kuwatambulisha Madaktari Diaspora aliofuatana nao.
Dr Ify Anne Nwabukwu akitowa Elimu ya tambua viashiria vya Saratani ya Matiti kwa wanafunzi hao wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar, Dr Ify akitowa mada kuhusiana na Saratani ya Matiti kwa Wanafunzi wa Chuo hicho hutoa Elimu ya Udaktari wa aima mbalimbali chuoni hapo.

Dr Ify akionesha Mashine ya kupimia Saratani ya Matiti ya Kisasa inayoitwa MamaGram hutumika kucunguza viashiria vya Saratani ya Matiti kwa Wanachuo hao wakati akitowa Elimu ya Saratani ya Matiti jinsi ya kumgundua Mwanamke mwenye matatizo hayo.Wanafunzi wa Chuo hicho wamepata fursa ya kuuliza mswali wakati wa Mafunzo hayo. Mmoja wa Madaktari hayo akitowa mfano hai kutokana na matatizo ya Saratani ya Matiti, kwa Wanachuo hao.

Daktari wa Meno Bi Queenate Ibeto akitowa elimu ya kutunza meno na kinga ya mane kwa Wanafunzi hao jinsi ya kuyatunza meno. wakati walipofika Chuoni hapo kutowa Elimu kwa Wanachuo hicho.  Daktari wa Meno Venessal Quitero akionesha moja ya tiba ya kunusuru meno kwa wanafunzi hao wakati wakitowa Elimu ya Utunzaji wa Meno na tiba yake. Mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar akionesha mafunzo ya utunzaji wa Meno kwa vitendo jinsi ya kupiga msuwaki inavyotakiwa kuweza kuimarisha meno kuwa imara

Dr Queenate Ibeto akionesha mfano ya vitendo kwa mmoja wa mnafunzi wa Chuo hichi jinsi ya utumiaji wa msuaki katika kupiga kwa Wanafunzi hao, wakati walipofika kutoa Elimu ya Afya kwa Wanafunzi wa Chuo hicho Mombasa Zanzibar. Profesa Hailu na Dr Quintero wakifuatilia Mada zilizokuwa zikiwakilishwa kuhusiana na Saratani ya Matiti na Tiba ya Meno, kwa Wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar Mombasa wakati walipofika katika Chuo hicho wakiwa Zanzibar kwa ajili ya kutoa Tiba ya Saratani ya Matiti Ugonjwa wa Kisukari na Meno.

Dr Quintero ni mtaalamu ya Magonjwa ya Meno akifafanua moja ya swali lililoulizwa na Wanafunzi wa Chuo hicho.Mwanafunzi wa chuo hicho akiuliza swali kuhusiana na baadhi ya Wananchi meno yao huwa na ukungu mweusi kwa wataalam hao Madaktari wa Diaspora wakigawa misuwaki na dawa za meno kwa wanafunzi hao baada ya kutowa Elimu chuoni hapo,

Dr Silvia Dasi akitowa maelezo kwa wanafunzi hau jinsi ya kumgundua mwanamke mwenye matatiti ya Saratani ya Matiti wakati wakifanya mafunzo hayo kwa wanafunzi hao wanaochukua Elimu ya Afya ya binadamu, Dr Silvia Dasi akitowa maelezo kwa wanafunzi hau jinsi ya kumgundua mwanamke mwenye matatiti ya Saratani ya Matiti wakati wakifanya mafunzo hayo kwa wanafunzi hao wanaochukua Elimu ya Afya ya binadamu,

Dr Ify akitowa Elimu ya Vitendo kugundua viashiria vya Saratani ya Matiti kwa Mwanamke akitowa mafunzo hayo ya mmoja wa mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar.
Dr Ify akitowa Elimu ya Vitendo kugundua viashiria vya Saratani ya Matiti kwa Mwanamke akitowa mafunzo hayo ya mmoja wa mwanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar kulia Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora Zanzibar Ndg Adila Hilal Vuai,

Madaktari Diaspora wakiwa katika picha ya kumbukumbu na Wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar baada ya kutoa Elimu kwao, DR Queenate Ibote akimfanyia uchunguzi wa meno mmoja wa wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar wakati walipofika Chuoni hapo kutowa Elimu kwa Wanachuo hicho.  DR Queenate Ibote akimfanyia uchunguzi wa meno mmoja wa wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar wakati walipofika Chuoni hapo kutowa Elimu kwa Wanachuo hicho. DR Queenate Ibote akimfanyia uchunguzi wa meno mmoja wa wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar wakati walipofika Chuoni hapo kutowa Elimu kwa Wanachuo hicho.
Madaktari wa Diaspora wakiwa katika picha ya pamoja na Wanafunzi wa Chuo cha Elimu ya Afya Zanzibar wakiwa nje ya jengo la Chuo hicho katika Skuli ya Sekondari ya SHAA Mombasa Zanzibar.
Picha na OthmanMapara.Blog Zanzinews.Com

No comments: