Saturday, 31 May 2014
Serikali ya Jubilee iko hatarini kukumbwa na African spring !
Muungano wa kisiasa wa upinzani nchini umeipa serikali makataa ya hadi tarehe saba mwezi julai mwaka huu kuandaa kongamano la kitaifa, la sivyo upinzani utazindua ratiba yake ya kutekeleza mabadiliko nchini.Muungano huo ukiongozwa na vinara wake Raila Odinga, Kalonzo Musyoka na Moses Wetangula umeikashifu serikali kwa kudai kwamba inatoa uongozi duni, na huenda upinzani ukawajibika kuchukua hatua kikatiba
.Hayo yamememwa katika bustani ya Uhuru wakati wa mkutano wa kisiasa wa kumkaribisha nchini kinara wa CORD Raila Odinga.
Friday, 30 May 2014
INTERVIEW WITH JOHN GITHONGO ABOUT KENYA CORRUPTION
Welcomes Kenyan Activist and Anti-Corruption Whistleblower John Githongo to Roundtable Discussion
1. In as few words as possible – and as simply as possible – tell us: What was Anglo Leasing all about?
Essentially the Government of Kenya entered into contracts – dubbed ‘security contracts’ which meant they could be single sourced.The ‘lease finance’ arrangements for these contracts purportedly approved by the cabinet meant that instead of the Government of Kenya going to suppliers directly for assorted goods and services, middlemen created companies which ‘lent’ money to the Kenyan government to purchase the goods.This happened even in cases where the countries from whom we were purchasing goods were willing to give us concessionary loans to purchase the goods because they recognised the business helped keep their citizens employed and those particular industries flourishing.
The provenance of these financing entities that the government entered into ‘contracts’ with were often dubious: they used false addresses, demonstrated absolutely no capacity to act as ‘financiers’, were determined to keep hidden who the beneficial owners of the entities were etc.Suspicions were heightened in 2004 when, after my office asked simple questions about these entities and the contracts they had been given, they proceeded to wire back the money (around US$12 million in total between May and August 2004) without revealing themselves to us or even complaining that their contracts had been ‘cancelled’. To this day it's still slightly grey who in the government picked up the phone and called who to get the money wired back. Unfortunately, some of the contracts (there were 18 contentious ones in total worth US$777 million) were aimed at delivering services and goods in the security sector that were intended at bolstering the infrastructure of fighting terror and enhancing security generally. And yet it was these contracts that seemed most inflated; where regard for quality was lowest and in some cases, no goods seemed to be delivered at all.
Thursday, 29 May 2014
Lesson From Malawi for Africa Leaders
"I learned that leadership is about falling in love with the people and the people falling in love with you. It is about serving the people with selflessness, with sacrifice and with the need to put the common good ahead of personal interests."These were the words of Joyce Banda, the president of Malawi, at the funeral of Nelson Mandela in South Africa last December, prompting one politician to remark: "She stole the show." Few who heard her inspiring tribute were likely to suspect that, six months later, Banda would be facing electoral humiliation, the end of her political career and potentially even jail.The results of Malawi's drawn out and chaotic election could finally be released as soon as Friday. Even if they are delayed again by the country's high court, it is widely believed that Peter Mutharika will be the winner while Banda, the second female head of state in Africa, will be the first to lose an election.
Here is the Unofficial results of Egyptian Presidential elections
And the unofficial Results of Egyptian presidential elections are here and there is no surprise
And the unofficial of results of the Egyptian presidential elections have been announced last night till early hours of morning and it is not big surprise : El-Sisi achieved a big landslide victory. Like all the military presidents of Egypt he scored over 96% according to the unofficial results published on Ahram Online. Exactly he scored 96.9% while his rival Hamdeen Sabahi achieved 3.1%. We expected this victory. The Field Marshal is a president elect now. Of course he will be declared official as president next 5 June “what a date” by EC.Military and the 90s percent … a love story since the 1960s in Egypt.
Wednesday, 28 May 2014
Kenyatta government surrender to CORD ?

Cord leader Raila Odinga (right), Kalonzo Musyoka and Moses Wetangula at a past rally in Kisumu. A confrontation between security forces and opposition supporters looms after Cord leaders swore to defy the government’s “cowardly” decision to ban political rallies in the city. PHOTO/FILE
A confrontation between security forces and opposition supporters looms after Cord leaders swore to defy the government’s “cowardly” decision to ban political rallies in the city.Cord insisted that a planned rally to welcome its leader Raila Odinga at Uhuru Park on Saturday is still on.The former Prime Minister has been in the United States for two months, on what has been described as a lecture tour.Police said they were banning all rallies for the forseeable future because of security fears.Madaraka Day is the same weekend and while the challenges of securing two big public events in a city under almost constant attack by terrorists are considerable, there are also suspicions in the opposition that the government is interfering with their rights.
Tuesday, 27 May 2014
The future of cash gate Lady Joice Banda

Instead, we’re trying to figure out what’s going on in a democracy that has done its level best this weekend to collapse in on itself, and take Malawi’s future with it.
The chaos began on Saturday, when President Joyce Banda – who has already rescued Malawi once before, remember, from the clutches of Bingu wa Mutharika’s budding autocracy – told the nation that she was riding to the rescue once again. Although she did not appear to have the constitutional authority to do so, she ordered the annulment of last week’s poll and scheduled a new election in 90 days’ time, insisting that the election had been so deeply flawed that she could not possibly inflict its results on the Malawian people.
So far, so stereotypical. It just so happened that Banda, with 30% of the vote counted, was trailing behind both Peter Mutharika (the late Bingu’s unexpectedly popular brother) and liberation party candidate Lazarus Chakwera. With her political future collapsing before her eyes, is anyone surprised that she would demand another chance?
This was far from a normal power grab, however. In fact, it was the opposite: Banda promised at the same time that she would not run in the new elections. “I have done this to allow that Malawians are given an opportunity to freely and fairly express their will in choosing their leaders in a free, fair, transparent and credible manner,” she said.
Saturday, 24 May 2014
Serikali ya Kikwete yapata Kiwewe cha mikutano ya UKAWA
Wakati Polisi mkoani Kigoma wakiwa wamemtia nguvuni Katibu Mkuu wa chama cha NCCR-Mageuzi, Mosena Nyambabe kwa tuhuma ya kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete, Kiongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), Profesa Ibrahimu Lipumba amesema hawatarudi bungeni mpaka kiongozi huyo wa nchi aombe radhi.Nyambabe alikamatwa juzi saa 5 usiku katika Kijiji cha Nguruka Wilaya ya Uvinza mkoani humo saa kadhaa baada ya kumalizika kwa mkutano wa hadhara wa UKAWA uliohutubiwa na Nyambabe na viongozi kutoka vyama vya Chadema na CUF.Akiwahutubia mamia ya wakazi wa Nguruka katika mkutano wa Ukawa wenye lengo la kuwaelimisha wananchi kuhusu mchakato wa Katiba, Nyambabe alisema Rasimu ya Katiba ikipita kuwa Katiba, mamlaka ya uteuzi wa ovyo haitakuwapo tena.“Jaji Warioba (aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba) ameweka mamlaka ya uteuzi kwenye Rasimu ya Katiba na Rais hataweza tena kuteua marafiki zake, shemeji zake, watu wake wa karibu kuwa viongozi mbalimbali hadi taratibu za ajira zifuatwe.“Hivi sasa kuna mawaziri mizigo walioteuliwa na Rais (Kikwete) ambao wanalalamikiwa na chama chake (CCM) kushindwa kutekeleza majukumu yao na hii inatokana na kupeana madaraka kwa njia zisizo stahili,” alisema Nyambabe.
Kikwete Government blamed for empty promises on 2010 Election campain.

Barely a year to the next general elections, unfulfilled election pledges by President Jakaya Kikwete during the 2010 now haunt Members of Parliament, many of whom are uncertain of their fate in the coming polls. Almost every legislator who took the floor to debate on the budget estimates expressed fear that the unfulfilled promises -- mainly on improving the condition of poor roads -- may cost fortunes in the next general election. In fact, some MPs said that voters could punish some of them for not doing enough to improve roads, and bring the president’s promises to reality. In particular, the MPs took issue with some ministers, saying they should be held responsible for the failure to ensure that the president’s pledges were fulfilled, more so because the elections are around the corner.
In his 2005 election campaign, the president promised to do the most he could to boost the national economy, in part, by pushing for the effective implementation of the national ‘Kilimo Kwanza’ initiative and further development of fishing industries and improve road infrastructure. He also vowed to continue empowering Tanzanians economically so that poor and marginalized wananchi could participate more actively and meaningfully in the country’s social and economic life.
Friday, 23 May 2014
Nigerian economy holds the key to ending hunger in Africa.

Nachilala Nkombo is Deputy Director - Africa at ONE.org Nigeria is not only Africa’s most highly populated country. As everyone now knows, with its recently rebased GDP of $500bn compared to South Africa’s $370.3bn at the end of 2013, the federal state has surpassed the latter as the continent’s largest economy
Jakob Zuma Kitchen cabinet

President Jacob Zuma’s decisions and appointments have largely been influenced by a “kitchen cabinet”, according to sources with intimate knowledge of how Zuma approached his first term of office.There is very little connection between members of this kitchen cabinet, and they are mainly located outside official ANC party structures.Three businesspeople have emerged as having played a key role in providing counsel to Zuma, particularly regarding major appointments.Businessman and playwright Duma Ndlovu, owner of Mvelase and Associates Vusi Mvelase, and executive chair of Zungu Investments Company Limited Sandile Zungu are said to influence Zuma’s decisions.
Ndlovu is said to have played a part in the appointment of national police commissioner Riah Phiyega as well as that of the former spokesperson in the presidency, Vincent Magwenya.
20 yrs of Black ruling in south Africa
No sooner had the final results of the recently concluded 2014 national elections been announced than President Zuma gave a predictably self-congratulatory speech lauding the result as “the will of all the people”. The reality however is that the ANC’s victory came from a distinct minority of “the people”. The real ‘winner’, as has been the case since the 2004 elections, was the stay away ‘vote’.Since South Africa’s first-ever democratic elections in 1994, the hard facts are that there has been a directly proportionate relationship between the overall decline in support for the ANC and the rise of the stay away ‘vote’. A quick look at the relevant percentages/numbers from each election confirms the reality.1994: Of the 23 063 910 eligible voters, 85,53 percent (19 726 610) voted while the remaining 14,47 percent (3 337 300) stayed away. The ANC received support from 53,01 percent (12 237 655) of the eligible voting population.1999: Of the 25 411 573 eligible voters, 62,87 percent (15 977 142) voted while the remaining 37,13 percent (9 434 431) stayed away. The ANC received support from 41,72 percent (10 601 330) of the eligible voting population.2004: Of the 27 994 712 eligible voters, 55,77 percent (15 612 671) voted while the remaining 44,23 percent (12 382 041) stayed away. The ANC received support from 38,87 percent (10 880 917) of the eligible voting population.2009: Of the 30 224 145 eligible voters, 59,29 percent (17 919 966) voted while the remaining 40,71 percent (12 304 179) stayed away. The ANC received support from 38,55 percent (11 650 748) of the eligible voting population.
Malawi election too close to call !
While Malawi election commissioner had accused the President of Malawi for demanding recount of the vote . Malawi Congress Party's (MCP) president Lazarus Chakwera and Democratic Progressive Party's (DPP) Peter Mutharika are almost equal from the 70 percent of the unofficial results in presidential election.Results from Blantyre, Mangochi, Nkhotakota, and Lilongwe City to complete the 30 percent will determine who wins.The other two contenders--incumbent President Joyce Banda of the People's Party (PP) and Atupele Muluzi of the United Democratic Front (UDF) - were on third and fourth positions respectively.
The results which were released for the past two days by the private Zodiak radio station - gave DPP leader, the brother of late President Bingu wa Mutharika, a narrow lead.But by Friday morning, other dispatched unofficial results at the tally centre indicated Chakwera was in frame to take the lead.The lead has come from Chakwera's strong showing in the south where he has been second to Peter in most votes counted.Mutharika has scored strongly in the south.Incumbent President Joyce Banda of PP was scoring highly in the Northern Region with United Democratic Front (UDF) candidate Atupele Muluzi performing fairly well in the Eastern Region districts of Zomba, Machinga and Mangochi.The Malawi Electoral Commission (MEC) are set to announce preliminary results on Friday.
Thursday, 22 May 2014
Malawi President lost election to Mutharika Brother
Malawi's President Joyce Banda on Thursday called for an immediate manual audit of this week's election results, alleging serious irregularities after the electoral commission reported its vote tallying system had collapsed."It has come to my attention that there (are) some serious irregularities in the counting and announcement of results in some parts of the country," she told reporters.Banda said unofficial partial results showed that some candidates were winning with numbers of votes that exceeded the total numbers registered at the polling centers.
Wednesday, 21 May 2014
Ukawa Watembelea Kaburi la Mwalimu Nyerere
Watanzania wametakiwa kuwa makini na watu wanaodaiwa kuwa wanafanya unafiki wa kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa maneno ya jukwaani, huku wakimnanga kwa kufanya vitendo vya kifisadi na ubadhirifu kinyume na mafundisho yake.Badala yake, hasa wakati huu ambapo taifa linapitia kwenye changamoto za kuandika Katiba Mpya, wananchi wametakiwa kumuenzi Baba wa Taifa kwa vitendo, kwa kupigania katiba mpya inayozingatia maoni ya wananchi kwa ajili ya maisha yao na hatma ya taifa.Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) alipoongoza msafara wa viongozi wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwenda kuzuru kaburi la Baba wa Taifa na kuijulia hali familia ya Mwalimu Nyerere, kijijini Mwitongo, Butima juzi, Jummane.Viongozi hao walipokelewa nyumbani kwa Mwalimu Nyerere na mmoja wa watoto wa familia hiyo, Madaraka Nyerere ambaye aliwatembeza katika kaburi la Hayati Baba wa Taifa, ambapo walipata fursa ya kuweka mashada ya maua katika kaburi hilo.Akiwakaribisha viongozi hao, Madaraka alisema kuwa pamoja na kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa mwanachama wa CCM, lakini familia hiyo inatunza hadhi yake ya kuwa Baba wa Taifa kwa kuwakaribisha watu mbalimbali hata kama ni wanachama au viongozi wa vyama vya upinzani, kutembelea kaburi hilo.Dkt. Slaa aliyekuwa ameongozana na Mjumbe wa Baraza Kuu la Chama cha Wananchi (CUF), Mustapha Wandwi na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha NCCR-Mageuzi, Hemed Msabaha pamoja na Kiongozi wa Shura ya Maimamu, Suweid Sadiq;
ODM party has relesed score card on Jubilee Government
The CORD coalition claims life under the Jubilee government has gotten worse for the ordinary citizen. In its report assessing the government's performance in the last year, the official opposition says Jubilee has implemented few, if any, of its electoral pledges.
Orange Democratic Movement has released a report card on the Jubilee government's performance in the past one year.In a statement sent to newsrooms by acting party leader Anyang' Nyong'o, ODM accused the government of not fulfilling its promises. "When the Jubilee Coalition took over power it promised Kenyans many things it has not fulfilled one year after being in office." read the statement. " Lap tops for school children: nothing. Digitalized government: nothing. Free maternity care for expecting mothers: grossly under funded. A place to feel at home in Kenya: we now live under perpetual insecurity. A unified and prosperous nation: divisive politics and the politics of exclusion continue to divide our people with Jubilee leaders as the chief architects of this " divide and rule politics," the statement read.
Orange Democratic Movement has released a report card on the Jubilee government's performance in the past one year.In a statement sent to newsrooms by acting party leader Anyang' Nyong'o, ODM accused the government of not fulfilling its promises. "When the Jubilee Coalition took over power it promised Kenyans many things it has not fulfilled one year after being in office." read the statement. " Lap tops for school children: nothing. Digitalized government: nothing. Free maternity care for expecting mothers: grossly under funded. A place to feel at home in Kenya: we now live under perpetual insecurity. A unified and prosperous nation: divisive politics and the politics of exclusion continue to divide our people with Jubilee leaders as the chief architects of this " divide and rule politics," the statement read.
Tuesday, 20 May 2014
President Kagame receives WTISD Award
President Kagame today received the 2014 World Telecommunication Information Society Award along with President Park Geun-Hye of Korea and Carlos Slim Helu, chairman of Grupo Carso and President of the Carlos Slim Foundation. The award is presented by the International Telecommunications Union (ITU) to individuals who have made exceptional contribution to improving lives of world citizens through ICTs.
In remarks following presentation of the award, President Kagame said:
“I want to express the sense of honour I feel in receiving this award. I do it in the humblest of ways knowing that this is an award of value that builds on the efforts of all Rwandans that have worked hard and embraced the policies and strategies of our development, that in a big part have been driven by ICT. This is the result of their efforts and progress and working together in our country, and also working notably with ITU that has been very supportive of efforts in Rwanda.”
Rais Joyce Banda akumbana na Wagombea 12 kwenye Kinyanga Nyiro cha urais nchini Malawi
Raia wa Malawi wanamchagua kiongozi wao katika Uchaguzi Mkuu
Raia wa Malawi wanapiga kura katika uchaguzi ulio na ushindani mkali, huku rais Joyce Banda,rais wa kwanza wa kike kusini mwa Afrika, akikabiliana na wagombea takriban 12, wanaowania kiti hicho cha urais.

Laini ndefu ya wapiga kura nchini Malawi Takriban watu milioni 7.5 zaidi ya asilimia 90 ya wananchi wamejiandikisha kupiga kura katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ilio na idadi ya watu milioni 16Banda anakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa wagombea wengine ikiwa ni pamoja na Peter Mutharika anayetokea chama cha DPP na ambaye ni nduguye rais wa zamani Bingu wa Mutharika pamoja na kasisi Lazarus Chakwera, kutoka chama cha Malawi Congress Party (MCP).Mgombea watatu kati ya 12 walio katika kinyanganyiro hicho cha kuwania urais ni Atupele Muluzi, mtoto wa rais wa zamani Bakili Muluzi, anayetokea chama cha
Sunday, 18 May 2014
Lema awakilisha mawazo ya Ukawa Bungeni leo

Mheshimiwa Spika,
Kwa mujibu wa ‘Instrument’ ya Serikali inayoainisha majukumu kila Wizara, Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi imepewa majukumu ya kushughulikia masuala ya Usalama wa Raia, Uhamiaji na utekelezaji wa Sera za zima moto na uokoaji. Aidha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inashugulikia pia masuala ya huduma za Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji, Uraia, Vitambulisho vya Taifa, Huduma za Wakimbizi, Usajili wa Vikundi au Vyama vya Kijamii, Huduma za Zima Moto na Uokoaji na mambo mengine yanayohusu maendeleo ya rasilimali watu katika Wizara hiyo.
Mheshimiwa Spika,
Ukitazama majukumu ya Wizara hii, utaona kwamba ina majukumu mazito sana yanayohusu usalama wetu sote kama raia wa nchi hii. Ni majukumu yanayohusu maisha yetu. Hivyo wizara hii inatakiwa iwezeshwe sana kibajeti ili iweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo ili wananchi na hata wageni waliopo katika nchi yetu waweze kuishi kwa usalama na amani. Kwa kuwa Wizara hii ina taasisi chini yake zinazohusika na ulinzi wa maisha ya watu na mali zao, hivyo ni Wizara inayotakiwa kufuatiliwa na kusimamiwa kwa karibu sana.
2. MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2013/2014
Mheshimiwa Spika,
Katika bajeti ya Wizara hii kwa mwaka wa fedha unaomalizika wa 2013/2014 Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni iliitaka Serikali kufanya mambo kadhaa ili kuboresha mapungufu tuliyoyaona katika katika kipindi hicho. Mambo hayo ni:
i. Kuchukua hatua kali na madhubuti ya kukabiliana na matukio yenye sura ya ugaidi kwa mfano kulipuliwa kwa bomu Kanisa Katoliki katika Parokia ya Olasiti huko Arusha, kuchomwa moto kwa makanisa huko Zanzibar na Dar es Salaam, Mapadre kuuwawa na Mashehe kumwagiwa tindikali Arusha na Zanzibar na matukio yanayofanana na hayo.
ii. Kuongeza posho ya chakula (Ration allowance) kwa askari wa Jeshi la Polisi ili walau posho hiyo ishabihiane na posho ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ili waweze kukabiliana na ugumu wa maisha. Kwa mujibu wa kumbukumbu rasmi za bunge (hansard) Waziri wa Fedha wa wakati huo Marehemu William Mgimwa alikubali posho ya chakula ya shilingi 225,000/= kwa mwezi kwa kila askari. Taarifa tulizo nazo ni kwamba posho hiyo haijalipwa mpaka leo. Je, askari waandike deni au wahesabu kwamba wamedhulimiwa?
iii. Kutoa mwongozo kwa maafisa wa Jeshil la Polisi na Magereza juu ya marekebisho ya sheria kuhusu umri wao wa kustaafu ambapo marekebisho ya sheria yaliongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 50 kwenda miaka 55 kwa maafisa wa Polisi na kutoka miaka 55 kwenda miaka 60 kwa akari wa Magereza.
iv. Kuondoa urasimu na utaratibu kandamizi katika Jeshi la Magereza kuhusu Mpango wa kujiendeleza kielimu kwa maafisa wa Magereza. Tuliitaka Serikali kufanya hivyo kwa kuwa, kwa mujibu wa General Service Order (GSO) na sheria nyingine za kazi, mtu akiajiriwa kwa mara ya kwanza (first appointment) na akataka kujiendeleza kimasomo nje ya kituo chake cha kazi anatakiwa kukaa kazini kwa muda wa miaka miwili au mitatu ndipo aweze kuomba ruhusa ya kwenda masomoni. Lakinini tulipokea malalamiko kutoka kwa maafisa wa Magereza kwamba sheria hiyo haifuatwi na badala yake maafisa hao wanatakiwa wakae miaka sita kazini ndipo wapewe kibali cha kujiendeleza kimasomo.
v. Kujenga nyumba za Askari wa Magereza ili kuboresha mazingira yao ya kazi na kuwafanya wasijisikie kama vile na wao ni wafungwa.
vi. Kuchukua hatua ya kupunguza msongamano wa wafungwa na mahabusu Magerezaji
vii. Kuboresha lishe na huduma za afya kwa Wafungwa na Mahabusu Magerezani
viii. Kuongeza fedha kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya zima moto na uokoaji kwa Jeshi la Zima Moto na Uokoaji
ix. Kuwachukulia hatua askari wa Jeshi la Polisi wenye vyeo vya juu wanaowanyanyasa askari wa vyeo vya chini.
x. Kuacha kulitumia Jeshi la Polisi vibaya kwa ajili ya kulinda maslahi ya kisiasa ya CCM
xi. Kuwachulia hatua kali za kisheria viongozi wa Jeshi la Polisi na viongozi wa Serikali waliotoa kauli za vitisho kwa waandishi wa habari walioandika habari za unyanyasaji unaofanywa na Jeshi la Polisi
xii. Kutoa ukomo wa muda ambapo kila raia wa Tanzania atapatiwa Kitambulisho chake cha Taifa na kuainisha ghrama zilizotumika katika mchakato wa kutengeneza vitambulisho vya Taifa.
xiii. ,Kudhibiti kuzagaa kwa silaha za moto ambazo hutumika katika matukio mengi ya kijambazi.
xiv. Kuchukua hatua kali kwa watu wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya hapa nchini
xv. Kuchukua hatua madhubuti za kupunguza matukio ya ajali barabarani ambayo yamepoteza maisha ya wananchi wengi sana wakiwemo polisi pia.
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kutoa taarifa ya utekelezaji wa masuala niliyoyataja hivi punde wakati wa majumuisho ya bajeti ya Wizara hii.
Mheshimiwa Spika,
Kwa mujibu wa Randama ya Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi fungu 51 na randama za taasisi zilizoko chini yake yaani Fungu 93(Idara ya Uhamiaji); fungu 28(Jesh la Polisi); fungu 29 (Magereza) na fungu 14 (Idara ya Zima Moto) hadi kufikia mwezi Machi, 2014 Wizara na taasisi zilipata mgawo wake wa kibajeti kwa wastani wa asilimia 70 isipokuwa idara ya zima moto na uokoaji ambayo ilipata asilimia 46.3 tu ya fedha zilizoidhinishwa. Aidha kwa Mujibu wa Randama ya Jeshi la Zimamoto, fungu 14 (uk. 2) katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/14 hakuna fedha yoyote iliyotengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa Jeshi la Zima Moto.
Mheshimiwa Spika,
Kwa mujibu wa Randama hiyo, huu ni mwaka wa tatu mfululizo kwa Jeshi la Zima Moto na Uokoaji kutotengewa fedha kwa ajili ya miradi ya Maendeleo. Kutokana na hali hiyo, Jeshi hilo limeshindwa kuendeleza ujenzi wa jengo la Ofisi ya Makao Makuu – TAZARA, Dar es Salaam, kushindwa kukarabati na kujenga vituo vipya vya zimamoto, kushindwa kununua vitendea kazi mbalimbali ikiwemo vifaa vya maokozi na vifaa vya kuzimia moto.
Mheshimiwa Spika,
Sote ni mashahidi wa majanga ya moto, maghorofa kuporomoka, meli kuzama, mafuriko na kila aina ya majanga ambapo idara ya zima moto imekuwa ikishindwa kufanya chochote na hivyo kuwaacha wananchi wakiangamia katika majanga hayo. Kambi Rasmi ya Upinzani inashawishika kuamini kwamba Serikali haina nia njema na usalama wa raia na ndio maana haitengi fedha hata senti moja katika miradi ya maendeleo ya Jeshi la Zima Moto. Kama Serikali haioni umuhimu wa Jeshi la Zima Moto ni bora kulifuta kuliko kuliacha wakati hailiwezeshi kufanya kazi yake.
3. HALI YA USALAMA NCHINI .
Mheshimiwa Spika ,
Hali ya Usalama Nchini imeendelea kuwa tete kutokana na sababu mbalimbali. Utafiti wa kiufuatiliaji uliofanywa na Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ni kwamba; sababu zifuatazo zinazorotesha hali ya usalama na amani hapa nchini.
i. Ukosefu wa Ajira na Kazi zenye Kipato kwa Jamii.
Mheshimiwa Spika,
Ukosefu wa kazi na ajira kwa Jamii umekuwa ni sababu moja ya msingi kabisa ya kuendelea kuhatarisha hali ya usalama na amani Nchini. Wananchi wengi hususan Vijana wamekuwa hawana uhakika wa ajira. Mbali na hofu na wasiwasi mkubwa walio nao, vijana hawa kutokana na kutojua hatima ya maisha yao, bado Serikali imeendelea kuwasakama katika shughuli zao ndogo ndogo. Kitendo cha Serikali kuwafukuza mijini vijana wajasiriamali wanaofanya biashara ndogondogo kumesababisha vijana hawa kushindwa kabisa kuweza kumudu hata mlo mmoja kwa siku. Jambo hili limewakatisha tamaa vijana wengi na matokeo yake ni kwamba baadhi yao wanajiingiza katika matukio ya kihalifu ili waweze kumudu maisha yao.
Mheshimiwa Spika,
Ili kujenga mazingira ya usalama, amani na utulivu katika nchi yetu, ni lazima sasa Serikali itambue wajibu wake wa kukuza uchumi na biashara kwa kasi ili kuongeza ajira na kazi zenye tija kwa jamii kwani kuachia Jeshi la Polisi kudhibiti hali ya ulinzi na usalama katika Taifa ambalo asilimia 80% ya Vijana wake wanarandaranda mitaani bila kuwa na kazi zenye uwezo wa kukidhi mahitaji yao muhimu ni hatari kubwa sio tu kwa walinzi hawa wa amani bali pia kwa taifa zima.
Mheshimiwa Spika,
Hivyo ni muhimu tukafahamu kwamba propaganda na tathimini feki kuhusu ukuaji wa uchumi zinazotelewa kila mwaka na Serikali wakati Watu wengi wanaendelea kuishi maisha yasiyo na matumaini na wengine wakishindwa kufurahia ajira na kazi kwa sababu ya masilahi duni na mfumuko wa bei za bidhaa unaosababishwa na uchumi kushuka kila mwaka, bila shaka sasa ni kweli kabisa kuwa hali ya usalama Tanzania ni tete na Jeshi Polisi haliwezi kujipanga kushindana na kundi kubwa la jamii iliyojaa hasira na kupoteza matumaini na maisha .
ii. Maslahi ya Askari wetu katika Muktadha wa Hali ya Usalama Nchini.
Mheshimiwa Spika,
Maisha ya Askari wa Jeshi la Polisi, Magereza, Zimamoto ni miongoni mwa kundi katika jamii ambalo linaishi maisha ya umasikini wa kupindukia sana. Nyumba zao, mishahara yao na masilahi yao mengine mbali mbali bado ni duni kiasi kwamba Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaona kuwa ni kebehi na dharau kubwa sana kwa vikosi vya ulinzi na usalama .
Mheshimiwa Spika,
Kazi ya Jeshi ni wito. Ni hatari kubwa sana kuwa na Askari ambao wanafanya kazi bila wito kwa sababu walikosa matumaini kwingineko, hivyo wakachagua kujiunga na Jeshi kama sehemu ya biashara.
Mheshimiwa Spika,
Ni ukweli usiopingika kuwa Askari wengi wanafanya kazi kwa moyo uliovunjika na kupondeka. Aidha, wana msongo mkubwa wa mawazo sababu ya ugumu wa maisha. Hali hii inaondoa uimara wa majeshi yetu haya kwani Jeshi imara sio tu kuwa na silaha za kisasa peke yake bali ni muhimu pia kuwa na askari wanaoona fahari kulinda raia na mali zao kama wajibu uliotukuka. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kutambua na kuthamini kazi inayofanywa na askari wetu ambao ni sehemu ndogo ya jamii iliyojitoa mhanga kufanya kazi za hatari hata kwa maisha yao ili kuwalinda raia na mali zao
iii. Rushwa na Uadilifu kwa Jeshi la Polisi
Mheshimiwa Spika,
Jeshi la Polisi limekuwa likitajwa kuwa kinara wa rushwa na chanzo cha biashara nyingi haramu. Jambo hili zio zuri hata kidogo kwa chombo kilichokabidhiwa jukumu la kuwalinda raia na mali zao. Hata hivyo, tafiti nyingi zinaonesha kwamba mazingira mabaya ya maisha yao yaliyojengwa katika maslahi duni ni miongoni mwa sababu zinazowasababisha kuingia katika tabia hii mbaya ambayo ni hatari kwa usalama wa Nchi .
Mheshimiwa Spika
Rushwa ndani ya Majeshi yetu ya ulinzi na usalama ni majaribu yanayo sababishwa na Serikali yetu. Hii ni kwa sababu mishahara na makazi ya askari wetu ni duni, vitendea kazi vichache na duni jambo linalochangia kwa kiasi kikubwa kuwa na askari wasio na
ari na shauku ya kazi ya ulinzi na usalama. Matokeo yake wanakosa nidhamu ya kazi na hivyo kujiingiza kwenye vitendo viovu ikiwemo rushwa na unyanyasaji wa raia. Ili kuwa na askari wenye nidhamu ya kazi, ni lazima kuwa na Serikali inayojua na kuthamini wajibu mkubwa wa vikosi vya ulinzi na usalama katika taifa. Kama vile Serikali inavyotoa mishahara mikubwa kwa wafanyakazi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)na Benki kuu ili kuwapa motisha wasiibe, vivyo hivyo Serikali ingeona umuhimu wa kuwalipa na kuwatunza vyema askari wa vikosi vya ulinzi na usalama kwa kuwa na askari wanaofanya kazi kwa moyo uliopondeka ni hatari kwa ukuaji wa uchumi na usitawi wa wananchi kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika,
Kitendo cha Serikali kupuuza maslahi mbalimbali ya askari wetu ni kuwaingiza katika majaribu mbalimbali ikiwemo rushwa, ukandamizaji na unyasaji dhidi ya raia wanaopaswa kuwalinda. Ifahamike kwamba kuwaingiza watu majaribuni ni dhambi. Aidha majaribu ya kumfanya mtu atende jambo baya yanahesabika kuwa ni dhambi. Ni katika muktadha huu, hata Bwana Yesu alipokuwa akiwafundisha wanafunzi wake kusali, aliwaambia wamwombe Mungu wakisema “….Usitutie Majaribuni bali utuokoe na Yule mwovu” Kwa hiyo Mheshimiwa Spika, Dhamira isiyokuwa na utu ya Serikali hii CCM juu ya usitawi wa nchi hii na watu wake ndio chanzo kikubwa cha askari wetu na wananchi wengine kuingia katika majaribu ya rushwa na aina mbalimbali za uhalifu.
Mheshimiwa Spika,
Ni kweli inawezekana kabisa binadamu akawa muadilifu bila kuwa na masilahi bora katika jamii, lakini vile ni ukweli usiopingika kwamba umasikini na hali duni ya maisha ndio unachangia kwa kiasi kikubwa kuondoa uadilifu na uimara wa nidhamu katika kukabiliana vishawishi vya rushwa na mambo mengine machafu yenye sura hizi.
Mheshimiwa Spika,
Kutokana na Serikali kuwa ndio mlezi wa rushwa, imekosa mamlaka ya kiuadilifu (moral authority) wa kukemea vitendo vya rushwa vinavyofanywa na taasisi mbalimbali zilizo chini yake. Kwa mfano kwa mujibu wa vyombo vya habari na kwa mujibu wa mjadala wa bajeti ya Serikali unaoendelea bungeni imeibuliwa kashfa ya wizi wa fedha zaidi ya shilingi bilioni 200 ambapo Viongozi Wakuu wa Serikali wamehusishwa. Katika jambo kama hili, Serikali inatoa wapi nguvu na sauti ya kukemea rushwa katika taasisi inazoziongoza kama vile jeshi la Polisi
.
Mheshimiwa Spika,
Kama wanaopaswa kukemea na kuzuia rushwa ni wala rushwa, ni wazi moja kwa moja kuwa, utamaduni wa kupokea rushwa na kula rushwa katika taasisi zote za Serikali ni jambo la Kawaida, na linaoipendeza Serikali ya CCM. Kwa hiyo, hakuna hata Kiongozi mmoja mwenye mamalaka ya kiuadilifu kukemea jambo hili, kwa kuwa familia zao zinaishi, zinasoma na kufurahia maisha kwa ajili ya ufisadi, wizi wa mali za Umma na rushwa .
Mheshimiwa Spika,
Kwa dhati kabisa, Kambi Rasmi ya Upinzani inaikemea Serikali kujenga mazingira ya rushwa kwa askari wetu. Kwa mfano kitendo cha Serikali hii ya CCM kukigeuza kitengo cha Askari wa Usalama Barabarani kuwa kitengo cha ukusanyaji mapato kwa makosa ya kutafutiwa na kulazimishiwa barabarani ni rushwa iliyowekewa mfumo rasmi. Jambo hili ni hatari sana kwa sababu rushwa ya aina hii haiwezi kumalizika kwa kuwa ina baraka za Serikali. Hali ni mbaya zaidi kwa kuwa katika kutekeleza jukumu hilo la askari kukusanya mapato, utaratibu umewekwa ambapo kila askari anatakiwa kutafuta kwa bidi, kulazimisha na kukamata makosa yasiyopungua sita mpaka tisa na kuyatoza faini. Mfumo huu mpya wa Serikali wa ukusanyaji wa mapato umeifanya rushwa barabarani kuwa rasmi.
Kambi Rasmi ya Upinzani inafahamu kwamba Serikali imeishiwa fedha, lakini tunaisihi sana isitumie njia za ukandamizaji na uonevu kujikusanyia mapato.
Mheshimiwa Spika,
Baada ya kuacha jukumu lao la msingi la kusimamia sheria za barabarani na kuanza kukusanya mapato, ajali za barabarani zimeongezeka sana. Kwa mujibu wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2013, jumla ya ajali za barabarani zilizohusisha magari katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya, Pwani, Kilimanjaro, Arusha na Morogoro zilikuwa ni 459,931, na ajali hizi zilisababisha vifo vya watu 2,408 na majeruhi 16,040. Kwa upande wa bodaboda watu waliofariki kutokana na ajali ni 1,106 na majeruhi 6,581.
Mheshimiwa Spika,
Ripoti ya Haki za Binadamu ya 2013, inasema kwamba nchi inapata hasara ya kati ya asilimia 1 hadi 2 ya Pato la Taifa (GDP) kutokana na ajali za barabarani. Kwa hiyo, uamuzi wa Serikali wa kukifanya kikosi cha usalama barabarani kuwa kitengo cha ukusanyaji mapato umekuwa ni hatari kubwa kwa maisha ya raia na uchumi wa nchi.
iv. Ukandamizaji, Ukatili na Uonevu Unaofanywa na Jeshi la Polisi.
Mheshimiwa Spika
Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya mahubusu kugoma kula , kuvua nguo hadharani na mambo mengine yakusikitisha ili kuonyesha hisia zao juu ya ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa dhidi yao. Madai makubwa ya mahabusu hao ni kwamba wanapata mateso makubwa gerezani kwa makosa ambayo wengi wao hawajayatenda. Hii maana yake ni kwamba Mahabusu wengi katika magereza yetu wamebambikizwa kesi jambo ambalo ni kinyume kabisa na utawala wa sheria na haki za binadamu.
Mheshimiwa Spika,
Ili kuondoa mwanya uliopo hivi sasa wa Polisi kuwabambikiza raia kesi na kuwaweka mahabusu, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali kufanyia marekebisho sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ili kuondoa fursa kwa baadhi ya askari wenye nia mbaya kutumia madaraka yao kuwabambikizia watu kesi kutokana na chuki au sababu nyingine. Kwa mfano, kijana mmoja wa Arusha, aliingia katika ugomvi wa mapenzi na askari polisi kwa sababu ya kumgombania binti. Askari yule alitengeneza mazingira kwa kijana yule kumbakiziwa kesi ya wizi wa kutumia silaha na mauaji na kuswekwa rumande. Kijana huyo wakati alipokuwa anaendelea kuteseka mahabusu, yule askari alimwoa mwoa yule binti. Baadaye askari huyo na binti huyo ambaye sasa ni mke wa yule askari wakaenda Magereza kumtembelea yule kijana aliyekuwa mahabusu kwa uonevu kama ishara ya kuonyesha umwamba!!!!!
Mheshimiwa Spika,
Mambo kama haya hayana idadi katika magereza zetu. Ni mengi. Uonevu na unyanyasaji unaofanywa na askari wetu katika kila kona ya nchi yetu ulijidhihirisha pia bomu lilipolipuliwa katika mkutano wa CHADEMA wakati wakuhitimisha kampeni za marudio ya Udiwani mwaka jana ambapo watu wanne walifariki Dunia na wengine wengi zaidi ya 100 kujeruhiwa vibaya wakiwemo watoto wadogo na Wanawake.
Mheshimiwa Spika,
Tuna ushaidi wa kutosha juu ya ni nani alihusika na mlipuko huo wa bomu. Licha ya kuwa baadhi ya polisi walihusika na mlipuko huo; Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ilimtaka Rais mara nyingi aunde tume ya Kijaji kwa ajili ya uchunguzi wa suala hili kubwa lakini hakufanya hivyo mpaka sasa. Badala yake kumekuwa na kejeli nyingi na mizaha juu ya suala hili hatari kwani waliokufa kwenye mkutano wa CHADEMA wanaonekana hawana tofauti na mbuzi au Kondoo.
Mheshimiwa Spika,
Sisi walengwa tuliotaka kuuwawa tunafahamu uchungu na mashaka tuliyo nayo dhidi ya maisha yetu. Hata hivyo mnaweza kuendelea kudharau jambo hili kwa sababu bado Utawala na Mamlaka yenu yanaendela kuelekeza, kupanga na kuendesha Nchi. Lakini jambo dhahiri ni kwamba; mateso haya, damu hizi, uonevu huu utafika mwisho na kama nyie hamtakuwepo basi watoto wenu watakuwepo na ndugu zenu wengine watakuwepo kushuhudia ukomo wa ukandamizaji, utesaji, uuaji na udhalimu huu dhidi ya raia wasio na hatia.
Mheshimiwa Spika,
Ni jambo la kusikitisha sana kwamba waliotaka kutuua pia waliendelea kupanga mipango ya kutubambikia kesi hiyo ya mauaji na ugaidi. Lakini Mungu akawa mwema, walikamatwa vijana wengi, wamepigwa, wameteswa na wengine sina uhakika kama wataweza kuwa na uwezo wa Nguvu za kuzaa tena tena kwa jinsi ya simulizi zao walivyofanyiwa ukatili wa ajabu na wote walilazimishwa kumtaja Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema viongozi waandamizi wa CHADEMA kuwa ndio waliohusika na mlipuko wa mabomu Kanisani Olasiti na kwenye Mkutano wa kufunga Kampeni za Udiwani za CHADEMA mwaka jana.
Mheshimiwa Spika ,
Katika vijana hawa waliopatiwa mateso makali baadhi yao walitolewa gerezani wakiwa na kesi nyingine na wakaelekezwa , wakapigwa , wakateswa na wengine kutishiwa kuuwawa wakubali kuwa mipango ya milipuko ya mabomu kanisani Olasiti na kwenye Mkutano wa CHADEMA yaliratibiwa na Mbunge wa Arusha Mjini na viongozi wakuu wa CHADEMA. Kwa tafsiri hii, inaonekana kwamba; waliolipua bomu katika Kanisa la Olasiti, ndio hao hao waliolipua bomu katika mkutano wa CHADEMA. Hii ni kwa sababu badala ya polisi kutawatafuta wahalifu hao na kuwashughulikia kwa mujibu wa sheria, wanahangaika kutafuta watu wa kuwabambikizia kesi kulipua bomu kanisani ili wawaunganishe na tukio la mlipuko wa bomu katika mkutano wa CHADEMA. Kwa sababu wanawatafuta watu wa kuwabambikiza kesi ni dhahiri kwamba Serikali inajua undani wa tukio hilo.
Mheshimiwa Spika,
Uadilifu wa Jeshi la Polisi umeendelea kuwa mashakani kwani baada ya Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki , Kijana mmoja Kiongozi wa CHADEMA wa Kata ya Usa river Msafiri Mbwambo aliuwawa kwa kuchinjwa shingo. Wauwaji wale walikamatwa na Jeshi la Polisi lakini cha kusikitisha ni kwamba baada ya muda mfupi wahalifu hawa waliweza kutoroka mbele ya Polisi kwenye chumba cha mahakama wakiwa wamefungwa pingu eti nakufanikiwa kumpora Askari Bunduki aina ya SMG na kukimbia nayo mpaka leo hawajaonekana wakiwa na pingu zao . Mheshimiwa Spika, huu ni upumbavu usiofikirika.
Mheshimiwa Spika
Hata wewe unaweza pia kuziba masikio yako kana kwamba hiki kinachosemwa ni “blues” na ngojera lakini Mungu yule unayemfuata Kanisani kila asubuhi kumuomba amesikia na yuko kazini . ‘Only Time will tell’.
Mheshimiwa Spika,
Kwa mujibu wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2013 (uk.22) watu 23 waliuwawa na vyombo vya dola kwa kipindi cha kuanzia Januari hadi Juni, 2013. Kuna mateso makubwa wanayopitia wananchi kutokana na uonevu wa askari wetu. Wanalia machozi mazito lakini hakuna msaada kwani Serikali inayopaswa kuwatazama na kuwalinda raia wake dhidi ya ukandamizaji huu , Serikali hiyo imepoteza ladha ya utu kwa hiyo kelele na mateso wanayopata Watu kwa kubambikiziwa kesi na kuwekwa mahabusu na kufungwa miaka mingi na kuuwawa, mateso hayo sasa yamegeuka kuwa laana kwa Nchi yetu.
v. Polisi Jamii
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani ina mtazamo kwamba ni vema kuwajengea wananchi utamaduni wa kuripoti matukio ya kihalifu kwa Jeshi la Polisi kuliko kuanzisha taasisi nyingine isiyo rasmi ndani ya Jeshi la Polisi. Tunatambua kwamba Jeshi la Polisi limeanzisha mfumo huu wa Ulinzi shirikishi kwa sababu ya uchache wa askari iliyo nao. Katika Randama ya Jeshi la Polisi, fungu 28, mojawapo ya changamoto zilizotajwa ni uchache wa askari Polisi. Kwa mujibu wa randama hiyo, idadi ya askari inayohitajika nchini kwa kiwango cha kimataifa ni 90,000 wakati waliopo sasa hawafiki nusu ya idadi hiyo. Aidha, Jeshi la Polisi linapata ugumu wa kupata taarifa za kihalifu kutoka kwa wananchi kwa sababu ya uadui uliojengeka kati ya wananchi na Jeshi la Polisi .
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni Bungeni inaitaka Serikali kuongeza ufanisi katika matumizi yake ya fedha, kuzuia ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma, kuwajengea wananchi uwezo wa kiuchumi ili fedha zitakazopatikana zitumike kuajiri askari ambao ni wataalamu wenye uwezo wa kuwalinda raia na mali zao badala ya kurasimisha mfumo usio rasmi wa polisi jamii ambao wengi wao ni green guards wa CCM.
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, inalaani Jeshi la Polisi kupuuzwa huko Zanzibar kwa kuvipa mamlaka zaidi dhidi ya Jeshi la Polisi vikosi vya KMKM, JKU na KVZ katika kusimamia shughuli za Ulinzi na Usalama wa Zanzibar. Jambo hili limeondoa mamlaka ya Jeshi la Polisi ambalo lina wajibu wa kulinda raia na mali zao katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
vi. Uchochezi wa Kidini na Kikabila
Mheshimiwa Spika,
Tatizo la udini na ukabila katika taifa hili linaonekana kuendelea kukomaa. Lakini ni tatizo ambalo halitamwacha hata mmoja wetu salama. Ni tatizo ambalo hakuna mshindi atakayepatikana. Ni tatizo ambalo hata kama litaisambaratisha nchi, hata wale watakaofanikiwa kuikimbia nchi hawatakuwa salama huko wanakokwenda kwa sababu watakuwa bado na imani zao na chuki hiyo dhidi imani nyingine itaendelea popote watakapokuwa.
Mheshimiwa Spika,
Kwa vile jambo hili linatishia usalama mpana wa taifa hili, ni vema sasa Serikali ikatafakari upya na kuleta sheria mpya itakayokataza na kuwawajibisha kwa nguvu zote wale wote watakaojaribu hata kwa maneno kueneza chuki au ubaguzi dhidi ya dini, kabila au rangi. Aidha, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka Serikali iombe radhi na kuwaondoa madarakani viongozi wote wa Serikali walitotoa kauli za uchochezi wa kidini, kikabila na rangi.
4. MAHUSIANO YA SERIKALI KATIKA BIASHARA HARAMU YA MADAWA YA KULEVYA NCHINI.
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, haina sababu ya kupoteza muda eneo hili kwani ni ukweli usiopingika kuwa biashara hii inafanywa na viongozi wakuu wa Serikali, hivyo basi waamue wao wenyewe kama wangependa kuendelea kuwa sehemu ya mateso na mauaji ya vijana wetu katika jamii ya watu inaowaongoza.
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani imelazimika kufikia uamuzi huu kwa kuwa viongozi wakuu wa nchi hii walishakiri hadharani kuwa wanawafahamu kwa majina watu wanaojishughulisha na biashara hii. Ni ajabu na ni kituko kama Rais wa Nchi ambaye ndiye amiri jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama anaogopa kuwataja wafanyabiashara haramu wa dawa za kulevya ambao alisema kuwa anawafahamu kwa majina. Tunashawishika kuamini kwamba bila shaka watu hao ambao mpaka Rais anagwaya kuwataja watakuwa ni malaika kutoka mbinguni au Mungu.
Mheshimiwa Spika,
Ni vema kama taifa tukatambua madhara ya madawa ya kulevya kwa vijana wetu ambao ndio nguvu kazi ya taifa. Kupuuzia na kutochukua hatua kwa wahusika wa dawa za kulevya ni kuangamiza nguvu kazi ya taifa. Nguvu kazi ya taifa ikishaharibiwa na dawa za kulevya hatuna taifa tena. Hivyo Serikali ifahamu kwamba kuendelea kulifumbia macho jambo hili ni kulihujumu taifa na huo ni usaliti mkubwa.
MAUAJI YA RAIA NA POLISI
Mheshimiwa Spika,
Toka mwaka 2011 katika hotuba zetu kuhusu Wizara hii tumeendelea kuonesha mauaji ya raia yanayofanywa na vyombo vya dola likiwemo Jeshi la Polisi. Wakati akihitimisha hoja yake hapa Bungeni Mhe. Waziri Mku Mizengo Pinda aliahidi mbele ya Bunge lako tukufu kuwa serikali ingeunda Mahakama ya Korona kwa ajili ya kuchunguza vifo hivyo kwa mujibu wa Sheria ya Uchunguzi wa vifo vyenye utata (Inquest Act).
Mheshimiwa Spika,
Serikali ilirudia kutoa ahadi ya kuanzisha Mahakama hiyo ya Korona kwa ajili ya kuchunguza vifo vilivyosababishwa na Operesheni ya kuondoa Majangili “Tokomeza” miezi michache iliyopita.
Mheshimiwa Spika,
Hadi leo ahadi hiyo ya Waziri Mkuu haijatekelezwa na badala yake Rais ameamua kuunda tume nyingine huku Bunge lako tukufu likiwa limewasilisha taarifa kuhusu Tokomeza jambo ambalo linaonesha serikali kutoamini taarifa ya Kamati ya Bunge lako tukufu.
Mheshimiwa Spika,
Kwa mwaka wa 2013 taarifa zinaonesha kuwa watu 23 waliuwawa na vyombo vya dola. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inamtaka Waziri mwenye dhamana ya Wizara hii kueleza Bunge lako tukufu juu ya kukithiri kwa tabia hii isiyokoma mwaka hadi mwaka na ni hatua gani zilizochukuliwa dhidi ya askari wanaohusika na mauaji haya.
Mheshimiwa Spika,
Aidha Kambi Rasmi ya Upinzani inamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya kuchukulia hali kama janga ndani ya Jeshi la Polisi na hivyo awe na mkakati wa kuzuia hali hii.
Mheshimiwa Spika,
Katika hali ya kushangaza hata wananchi wameanza kuchukua sheria mkononi kwa kuwadhuru na hata kuwaua askari polisi. Kwa mwaka 2013 vituo vya polisi takribani vitano vilivamiwa na wananchi na mali kadhaa za Jeshi hilo kuharibiwa, aidha vifo kadhaa vya askari viliripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Spika,
Kama matukio hayo hayatoshi wananchi kwa makundi yao katika maeneo mbalimbali ya nchi walizidi kujichukulia sheria mkononi kwa kuwaua watu mbalimbali ambao wametuhumiwa kufanya makosa ya jinai kama vile wizi. Kwa mwaka jana pekee watu 1669 waliuwawa[1].
Mheshimiwa Spika,
Upo uhalifu mwingine ambao umejitokeza katika nchi yetu ambapo watu wamekuwa wakizikwa wakiwa hai. Matukio kama ya hayo yametokea katika Wilaya Chunya na maeneo mengine katika Mkoa Mbeya.
Mheshimiwa Spika,
Hali hii ya mauaji ya raia yanayofanywa na vyombo vya dola na pia mauaji yanayofanywa na wananchi kwa wahalifu na pia kuvamia na hata kuua Polisi sio jambo la kulifanyia mzaha kabisa. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inaitaka serikali kuchukua hatua za dharura na kutoa taarifa Bungeni na bila kufanya hivyo italazimika kuamini kuwa serikali iliyopo madarakani imetoa Baraka kuhusu vitendo hivi vya kinyama kuendelea kutokea katika nchi yetu.
5. UHAMIAJI HARAMU NA USALAMA KATIKA MIPAKA YA NCHI YETU
Mheshimiwa Spika,
Mipaka ya Tanzania haipo salama kabisa kwa sababu imeendelea kuwa kichaka kwa wahamiaji haramu. Hali hiyo pia inathibitika na kile kilichosemwa na Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmi Bungeni katika Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kuhusu kung’olewa kwa alama (beacons) za mipaka yetu katika maeneo mbalimbali nchini. Hata hivyo, mahusiano mabaya ya Tanzania na baadhi ya jirani zake yanafanya hali ya usalama mipakani kuwa ya hatari zaidi. Kwa mfano, kumekuwa na mvutano kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame kwa mujibu wa vyombo vya habari. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inahoji, kutofautiana kwa maneno kati ya Rais Kikwete na Kagame kunatosha kuwa ugomvi kati ya nchi hizi mbili kwani hili lisipotazamwa vizuri linaweza kufifisha matumani ya wananchi wa nchi hizi mbili kuishi kama ndugu ndani na nje ya mipaka yetu.
Mheshimiwa Spika,
Tanzania imejaa wageni wengi kutoka nchi mbalimbali kama vile Bangladesh, India, China, Pakistan, na nchi nyingene za Afrika na Afrika Mashariki wanaofanya kazi hapa nchini katika fani na taaluma ambazo watu wetu wanazo. Kambi Rasmi ya Upinzani inahoji kama ni sera ya Serikali hii ya CCM kutoa kipaumbele cha ajira kwa wageni katika fani, ujuzi na taaluma ambazo watanzania wanazo. Aidha, tunaitaka serikali kupitia idara ya uhamiaji na idara nyingine za serikali kupitia takwimu za wageni waliopo nchini na shughuli wanazozifanya ili kuona kama wageni hao wana uhalali wa kuendelea kuwepo na kufanya kazi nchini ikiwa hakuna kazi inayohitaji taaluma maalumu (special skills) ambazo watu wetu hawana.
6. HITIMISHO
Mheshimiwa Spika,
Kila aliyepata fursa ya kusikiliza kwa makini maoni haya ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni angetaka kuona tunatoa suluhisho gani juu ya nini kifanyike kuhusu mambo haya. Hata sisi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni tunafikiri ni vyema kushauri na kusaidia kuonyesha njia muafaka ili kuliokoa taifa letu na mateso haya, lakini tunapata wakati mgumu kuishauri Serikali ambayo imepoteza thamani ya utu dhidi ya watu wake. Hivyo basi, kama kuna mambo ya kushauri, basi tungeshauri yafuatayo
Moja: Mungu asaidie Serikali hii ya CCM iondoke madarakani mapema kabla haijaharibu mfumo wa kumpata kiongozi kwa njia ya demokrasia kwani hali ikiendelea hivi; iko siku watu wataingia barabarani. Hali hii tayari imeshaanza kujitokeza kwani mwaka Kwa kipindi cha Januari hadi Desemba 2013 pekee watu 1669 waliuwawa kwa sababu ya watu kujichukulia sheria mkononi. Tunajua watu watakapojitokeza kudai haki zao na kupinga uonevu watapigwa mabomu ya machozi, risasi, na vitisho na mateso mbali mbali lakini tunajua hawatarudi nyuma; kwani watakuwa wamedhamiria kujitetea na kuwatetea ndugu zao na nchi yao dhidi ya mateso, ukandamizaji, uonevu na dhiki inayotokana na mambo hayo. Kinyume chake, yatakapotokea hayo, Serikali itakuwa imetangaza ukomo wa utawala wa kidemokrasia na hilo linaweza kuwa chimbuko la machafuko na umwagaji damu, hivyo ni vyema waumini wa imani mbalimbali wafanye dua na sala ili Serikali hii ya CCM iondoshwe madarakani katika uchaguzi mkuu ujao kwa amani.
Pili: Siku Serikali hii ya CCM ikijua kuwa nguvu ya Mfalme ni watu na sio bunduki na mabomu ya machozi, siku hiyo ndipo mtakapoanza kupata hekima ya kuheshimu utu wa binadamu na kile kinachoonekana sasa kama mateso, udhalimu na ukandamizaji vinaweza kurekebishwa.
Tatu: Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kutambua kuwa heshima ya kiongozi haijengwi kwa uwezo wa mali wala utawala bali katika kazi njema, heshima, utu, na upendo. Ikiwa Serikali itaelewa hivyo; basi wajibu wake katika kutafuta na kupigania maisha ya mtu mmoja mnyonge anayeteswa na kudhalilishwa itakuwa ndio hazina na heshima kubwa kwa viongozi wa serikali na taifa kwa jumla.
Mwisho: Tunafahamu kwamba ndani ya Serikali kuna watu wengi waadilifu na wenye dhamira njema na nchi yetu. Hata hivyo, wanashindwa kuchukua uamuzi wa kukemea uovu kutokana na utamaduni wa Serikili kuwatisha na kuwawekea vikwazo mbalimbali watu wa namna hiyo. Kutokana na hali hiyo, jamii yetu imejengwa katika fikra za hofu na woga kwa mambo ambayo yanahitaji uamuzi thabiti na kauli za kijasiri ili kulinusuru taifa na maangamizi.
Mheshimiwa Spika,
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inataka Serikali ijue na wananchi wote wajue kwamba; “Dhambi mbaya na kubwa kuliko zote Duniani ni woga”. Hivyo Basi Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inawaasa viongozi wachache wenye dhamira njema kwamba waache woga wasimamie misingi ya haki na ukweli hata kama gharama zake ni Maisha yao kwani msingi wa Taifa letu la kesho unajengwa na viongozi na utawala ulioko madarakani leo.
Mheshimiwa Spika,
Baada ya kusema hayo, kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, naomba kuwasilisha
Godbless Jonathan Lema (Mb)
MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI NA
WAZIRI KIVULI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Source: Dira yetu blog
Lema awakilisha mawazo ya Ukawa Bungeni leo
Friday, 16 May 2014
Lema awakilisha mawazo ya Ukawa Bungeni leo
HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI
BUNGENI, MHE.GODBLESS JONATHAN LEMA (MB), AKIWASILISHA BUNGENI MAONI YA KAMBI
RASMI YA UPINZANI BUNGENI KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2013/2014
NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI KWA
MWAKA WA FEDHA 2014/2015.
1.
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Kwa mujibu wa ‘Instrument’ ya Serikali inayoainisha
majukumu kila Wizara, Wizara ya Mambo ya ndani ya Nchi imepewa majukumu ya
kushughulikia masuala ya Usalama wa Raia, Uhamiaji na utekelezaji wa Sera za
zima moto na uokoaji. Aidha Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi inashugulikia pia
masuala ya huduma za Jeshi la Polisi, Magereza, Uhamiaji, Uraia, Vitambulisho
vya Taifa, Huduma za Wakimbizi, Usajili wa Vikundi au Vyama vya Kijamii, Huduma
za Zima Moto na Uokoaji na mambo mengine yanayohusu maendeleo ya rasilimali
watu katika Wizara hiyo.
Tuesday, 13 May 2014
SERKALI YA CCM YATAKIWA KUONESHA ZILIPO MAITI YA ALIEKUWA WAZIRI MKUU WA ZANZIBAR

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan alikataa kueleza walipo waasisi sita wa Muungano ambao kambi ya upinzani ilidai kuwa waliuawa na kuzikwa handaki moja, badala yake akatumia nafasi hiyo kumshambulia mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu akidai hizo ni propaganda na upotoshaji.
Juzi wakati akiwasilisha hotuba ya Kambi Rasmi ya Upinzani, Lissu aliitaka Serikali kutoa maelezo bungeni kuhusu sababu za kuuawa kwa waasisi sita wa Muungano wa Tangayika na Zanzibar na kuzikwa katika handaki moja visiwani Zanzibar. Lissu aliwataja waasisi hao kuwa ni Abdalah Kassim Hanga, aliyekuwa waziri mkuu, Abdul Aziz Twalam aliyekuwa Waziri wa Fedha na Abdulaziz na Saleh Akida aliyekuwa mjumbe wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar.
Pia aliwataja Othman Shariff, Mdungi Ussi na Jaha Ubwa ambao alisema nao waliuawa na kuzikwa katika handaki moja eneo la Kama nje kidogo ya Zanzibar.“Tunataka kujua ukweli kama walifanya makosa, walishtakiwa katika mahakama gani iliyowahukumu adhabu ya kifo... tunataka kuambiwa ukweli kwanini mchango wao kuhusu Muungano umefichwa,” alisema Lissu juzi. Lakini alipoulizwa kuhusu madai hayo, Waziri Hassan alionekana kuzigeuza hoja hizo kuwa ni za Lissu pekee badala ya kambi ya upinzani na kumshambulia mbunge huyo akidai kuwa ni mpotoshaji, anayepiga propaganda na mchochezi.
Waziri huyo, ambaye ni Mzanzibari, alisema alipuuza maswali yote kuhusu waasisi hao akisema mbunge huyo wa Chadema alipotoka katika hotuba yake na ndio maana hakutaka kuzungumzia katika majumuisho ya bajeti ya ofisi yake bungeni.“Yule Lissu sio mkweli na ndio maana sisi tulimpuuza,” alisema waziri huyo. “Hakuna kitu kama hicho na endapo kingekuwepo sisi Serikali tungeshatoa ufafanuzi ili watu wapate kujua ukweli wake,” aliongeza Waziri Samia bila kutoa ufafanuzi wa nini kiliwatokea watu hao walioshika nafasi za juu serikalini mara baada ya Mapinduzi na Muungano wa Zanzibar na Tanganyika. Pamoja na kudai kuwa aliona hoja hizo ni upotoshaji, Waziri huyo, ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba, aliwasihi wabunge wa upinzani kupeleka hoja zao katika Bunge Maalumu la Katiba linalojadili uundwaji wa Katiba Mpya, ambalo pia limetawaliwa na suala la muundo wa Muungano na kero zake.Waziri Samia alisema hoja hizo zinalenga kuwaaminisha Watanzania mambo ambayo hayapo ili kuwajaza chuki dhidi ya Serikali yao na pia alidai zina uchochezi ndani yake. Waziri Samia aliwashauri wabunge pamoja na Watanzania kupuuza kauli hizo akidai mbunge huyo hautakii mema Muungano na ndio maana anaibua mambo aliyodai kuwa ni ya uongo na ya uchochezi .
Lissu alitoa madai hayo akinukuu kitabu cha Kwaheri Ukoloni, Kwaheri Uhuru kilichoandikwa na Harith Ghassany ambacho kinaonyesha jinsi ambavyo viongozi hao wa SMZ waliuawa na kuzikwa katika kaburi moja.
“Sisi wa kizazi cha Muungano tunataka kujua ukweli juu ya makosa waliyoyafanya hawa waasisi wa Muungano hadi wakauawa na kuzikwa katika kaburi au handaki moja,” alisema Lissu. Jitihada za kumpata Makamu wa Pili wa Rais wa SMZ, Balozi Seif Ali Idd na Waziri wa Nchi katika ofisi yake, Mohamed Abood kuzungumzia msimamo wa SMZ kuhusu kauli hiyo hazikuzaa matunda kwa kuwa simu zao ziliita bila majibu. Akizungumzia suala hilo, mbunge wa viti maalumu, Anna Abdallah alisema naye alidai hoja hizo za Lissu ni za uchochezi ambao usipopuuzwa, unaweza kusababisha chuki kwa jamii. “Ule ulikuwa ni uchochezi, na upinzani wa aina hiyo ni wa ajabu sana… kwa mtazamo wake yeye anafikiri anawafurahisha Wazanzibari, lakini wamemuona ni mtu wa ajabu,” alisema mwanasiasa huyo mkongwe. Pamoja na uzito wa tuhuma hizo, baadhi ya wabunge waliohojiwa na gazeti hili jana walionekana kuzungumza kimkakati kwamba hawakusikiliza hotuba hiyo. Utata mkubwa bado umezunguka kutoweka kwa Hanga na wenzake machapisho mbalimbali yanawatambua kama watu waliokuwa mstari wa mbele katika Mapinduzi ya Zanzibar na ambao
LISSU SPEAK FOR ZANZIBAR
The National Assembly has been asked to form a Select Committee to oversee distribution of ‘Union funds’ received through budgetary grants and loans and to also make public the distribution criteria.
Shadow Minister of State, Vice President Office in charge of Justice, Constitution and Union Affairs Tundu Lissu made the call yesterday in parliament. Tabling alternative budget estimates for the 2014/15 financial year for the vice president office (Union and Environment) the outspoken Singinda MP said the suggested committee would among other things make known the amount that the Isles are expected to receive as direct donation from development partners contributing to the Union government basket fund. He told the House that during the last financial year, Tanzania’s total revenue resulting from soft loans and grants from donors amounted to 1.163trn/- but Zanzibar received only 32.62bn/- instead of the required 52.33bn/-.
“Under this clause, Tanzania Mainland obstructed 25.14bn/- …the legal amount which was supposed to be paid to Zanzibar and during the financial year 2014/15 Zanzibar will receive only 21.6bn/- out of 992.17bn/-,” he claimed.“It’s not only that Zanzibar is not benefiting from revenue generated as soft loans and grants to the union government, but it also does not benefit from revenue collected from union matters,” he alleged. The legislator further questioned why the government had failed to implement the Mutual Fund Act of 2003 that calls for among other things, establishment of a commission to oversee the mutual fund. Lissu went on to allege that Union revenues surpass Union demands yet only a small amount is allocated to deal with union issues while, according to him, a lot of money is commissioned to issues not related to Union matters. The Legislator also asked the government to make public the whereabouts of principal founding leaders of the Union from both the Isles and the Mainland. These he named as Abdallah Kassim Hanga, Abdullaziz twala and Saleh Saadalla Akida from Zanzibar and Oscar Kambona, Bhoke Munanka and Job Lusinde from Tanganyika.
NEW BLOOD IN MOZAMBICAN POLITICAL SYSTEM
Daviz Mbepo Simango (born February 7, 1964) is a Mozambican politician, the President of the Democratic Movement of Mozambique (MDM) and the current mayor of Beira. He is son of Uria Simango, the first Vice-President of FRELIMO. He joined the RENAMO in 1997 and became the mayor of Beira in 2003 as its candidate. On March 6, 2009, he founded a new party, the MDM.Mozambique will hold national elections in October. Politics in the southern African nation has been dominated by two parties, FRELIMO and RENAMO. But now a young party is causing waves across the country, pledging to focus on ‘a development agenda’
In 2009 Mozambicans watched the birth of a new political party, the Democratic Movement of Mozambique (Movimento Democrático de Moçambique – MDM). In only four years the party has managed to gain control of three strategic municipalities. In the last municipal elections in 2013, it emerged as a serious challenger to the ruling FRELIMO, one year ahead of the national elections. Meanwhile, very little is known about MDM’s political orientation and the reasons behind its rise. To gain greater insight into MDM’s political thinking, Fredson Guilengue, project manager at the Rosa Luxemburg Stiftung – Southern Africa (RLS), interviewed the head of the national parliamentary group of MDM, Lutero Chimbirombiro Simango (LS). Lutero was born in 1960 and is the older brother of Daviz Simango, president of MDM. While Daviz [2] resides in Beira, Lutero is based in the capital city of Maputo. Their parents Uria and Celina Simango were assassinated. [3] Uria Simango was one of the founding members of FRELIMO and its vice president from the party’s inception in 1962 until the time of the assassination of its first president Eduardo Mondlane in February 1969. He was then ousted in an internal power struggle in which Samora Machel and Marcelino Dos Santos took control of the party.
Monday, 12 May 2014
UKAWA ISSUE SCHEDULE FOR THERE COUNTRY WIDE RALLY

The Coalition of Defenders of People’s Constitution (Ukawa) yesterday issued the schedule for their countrywide public rallies aimed at creating awareness on the ongoing Constitution-making process.
According to the timetable, the meetings, which will be preceded by peaceful demonstrations, will start on May 14 to May 27, encompassing three major zones: Northern Zone, Central Zone and Southern Highlands Zone.The aim of the rallies, according to Dr Willibroad Slaa, the Chadema secretary general, is to provide education to the public over the ongoing Katiba making process that has culminated in a tug-of-war between the proponents of three-government and two-government systems.Speaking in Dar es Salaam yesterday, Dr Slaa said Ukawa outside the Parliament are determined to make sure the new Constitution the country will have, will adhere to citizens’ opinions, “unlike those being advocated by the ruling CCM.”The three zones, according to Mr Julius Mtatiro, the deputy secretary general of CUF, will be led by three opposition political heavyweights including Mr Mosena Nyambade (NCCR Mageuzi –Secretary general) in the Central Zone, assisted by two members - Ashura Mustafa (CUF) and John Heche (Chadema). Dr Slaa will take the lead in the Northern Zone assisted by Mr Mustafa Wandwi (CUF) and Mr Ahmed Msabaha (NCCR-Mageuzi). The Southern Highlands Zone will be led by Prof Ibrahim Lipumba, the CUF chairman, assisted by Mr Said Issa (Chadema) and Mr Martin Danda.
“We will have public rallies countrywide. These will be preceded by peaceful demonstrations. We’d like to urge the police and other coercive instruments not to interfere with these meetings. They need to treat us as they have been treating CCM meetings, ” said Dr Slaa. Dr Slaa added: “Ukawa is here to stay.Its members are working collaboratively to make sure that the Constitution of the people is obtained. It is just too bad for those who believe that Ukawa is a mere passing cloud.”Mr Mtatiro said Tanzanians should be aware that after finishing the Katiba-making process, the next task will be the Constitution building process.“If we will do a mistake by letting one political party drive its agenda on behalf of the public, we are not going to have a people-centered constitution,” said Mr Mtatiro
MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI OFISI YA MAKAMO WA RAIS
MAONI YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO), MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU (MB.) KUHUSU MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA FEDHA YA OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO) KWA MWAKA 2014/2015
(Kanuni ya 99(9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013)
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
Mwaka huu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imefikisha umri wa nusu karne tangu ilipozaliwa tarehe 26 Aprili, 1964. Kama anavyosema Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda katika hotuba yake ya tarehe 7 Mei, 2014 ‘Kuhusu Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio ya Matumizi ya Fedha ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa Mwaka 2014/2015’: “Miaka 50 kwa lugha yoyote ile siyo kipindi kifupi.” Waziri Mkuu ametumia takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 zinazoonyesha
kwamba asilimia 90.6 ya Watanzania wote “wamezaliwa ndani ya Muungano na nchi wanayoifahamu ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.” Kwa maneno ya Waziri Mkuu, “sote tunawajibika kuwatendea haki watu hawa kwa kuulinda, kuuimarisha na kuudumisha Muungano wetu.”
Mheshimiwa Spika,
Kama ilivyo kwa Watanzania wengine wengi, na mimi pia nimezaliwa ndani ya Muungano. Ninaamini kwamba ukweli huu unawahusu pia waheshimiwa wabunge wengi waliomo ndani ya Bunge hili tukufu. Na sisi pia tunaomba kutendewa haki kuhusu Muungano huu. Hata hivyo, Mheshimiwa Spika, haki tunayoomba Page 2 of 27 kutendewa ni moja tu: kuambiwa ukweli juu ya Muungano huu na historia yake, hali yake ya sasa na mwelekeo wake wa baadaye. Haki tunayoomba kutendewa ni kwa watawala kuacha propaganda na uongo juu ya Muungano na kutuambia ukweli wote juu ya Muungano huu. Bob Marley, aliyekuwa mwanamuziki mpigania uhuru wa watu weusi maarufu kutoka Jamaica, aliwahi kusema katika wimbo wake ‘Get Up, Stand UP, Stand Up For Your Rights’ (‘Amkeni, Simameni, Simameni kwa Haki Zenu’) kwamba: “You can fool some people some time, but you cannot fool all the people all the time”, yaani, unaweza kuwadanganya baadhi ya watu kwa muda fulani, lakini huwezi kuwadanganya watu wote kwa muda wote! Baada ya nusu karne ya uongo na propaganda kuhusu Muungano huu, Watanzania wa kizazi hiki cha Muungano wanataka ukweli. Na Watanzania hawa hawataulinda, wala kuuimarisha au kuudumisha Muungano huu endapo wataendelea kudanganywa au kufichwa ukweli juu ya mambo mengi yanayouhusu. Kwa hiyo, Mheshimiwa Spika, sisi kizazi cha Muungano tunahitaji kutendewa haki: acheni propaganda na uongo kuhusu Muungano huu ndipo muweze kutuambia tuulinde, tuuimarishe na tuudumishe!
Saturday, 10 May 2014
UKAWA WATANGANZA BARAZA LA MAWAZIRI
Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, ametangaza Baraza lake la mawaziri kivuli 28 na naibu mawaziri 12, na kufanya baraza lote kuwa na mawaziri 40.
Katika baraza hilo la mawaziri linalojumuisha wabunge wanaotokana na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), mawaziri 25 wanatoka Chadema, 11 wanatoka CUF na NCCR-Mageuzi ni wanne.Mawaziri kivuli walioachwa katika baraza hilo ni Sylvester Kasulumbay (Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi), Highness Kiwia (Viwanda na Biashara) na Rose Kamili (Kilimo, Chakula na Ushirika).
Wengine walioachwa na Mbowe akasisitiza kuachwa kwao siyo kwa sababu hawawezi kazi bali ni kutaka kuwa na baraza la mawaziri dogo ni Sabrina Sunga (Naibu Waziri Maji).Katika Baraza hilo, nafasi ya mnadhimu mkuu wa upinzani Bungeni iliyokuwa ikishikiliwa na Tundu Lissu (Chadema) sasa itashikiliwa na Mbunge wa Tumbe, Rashid Abdalah kutoka chama cha CUF.
Akitangaza baraza hilo Bungeni mjini Dodoma jana, Mbowe alisema Wizara ya Katiba na Sheria imeongezewa majukumu ya Muungano na waziri wake atakuwa ni Lissu na naibu wake ni Abdalah.Pia amemteua Mbunge wa kuteuliwa na Rais ambaye pia ni Mwenyekiti wa taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia ambaye anakuwa Waziri wa Fedha wakati Naibu wake atakuwa Christina Lissu kutoka Chadema. Mawaziri Ofisi ya Rais ni Profesa Kulikoyela Kahigi (Utawala Bora-Chadema), Vicent Nyerere (Utumishi-Chadema) na Esther Matiko (Mahusiano na Uratibu-Chadema).Ofisi ya makamu wa Rais itakuwa na mawaziri wawili ambao ni mchungaji Israel Natse kutoka Chadema atakayeshughulika na Mazingira na Naibu wake atakuwa ni Assah Othman Hamad (CUF).Mnadhimu wa Upinzani Bungeni ndiye atakayeshikilia pia nafasi ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais anayeshughulikia Mazingira.
Subscribe to:
Posts (Atom)